Home » » WAZIRI WA NISHATI NA MADINI ATEMBELEA BWAWA LA KUZALISHA UMEME LA MTERA

WAZIRI WA NISHATI NA MADINI ATEMBELEA BWAWA LA KUZALISHA UMEME LA MTERA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Na. bilson vedastus - Dodoma
Naibu Waziri Nishati na Madini anayeshughulikia masuala ya Nishati Mhe. Charles Kitwanga amefanya ziara ya kutembelea Bwawa la kuzalisha Umeme la Mtera mwishoni mwa wiki kwa lengo la kuangalia mwenendo wa maji katika bwawa hilo. 
Wakati akizungumza na watendaji wa Bwawa hilo, Kitwanga amewataka watendaji hao kuhakikisha kuwa Bwawa la Mtera linaendelea kuwa na kiasi cha maji ya kutosha wakati wote ili kuweza kuzalisha umeme wa kutosha.
Aidha, ameongeza kuwa, uzalishaji umeme kwa njia ya maji ni muhimu kutokana na gharama zake kuwa nafuu ikilinganishwa na gharama za kuzalisha umeme unatokana na gesi au vyanzo vingine. Hivyo, amewataka wananchi wanaofanya shughuli zao jirani na vyanzo vya maji kuhakikisha wanavilinda kwa ajili ya maendeleo na manufaa ya taifa.
Katika hatua nyingine amewataka watendaji hao kufikiria vyanzo vingine vya kuzalisha umeme mbali na gesi badala ya kusubiri rasilimali ya gesi pekee kuweza kuzalisha umeme.
Aidha ameeleza kuwa, wananchi wana matarajio makubwa na nishati ya umeme hivyo, amewataka watumishi wa Wizara ya Nishati na Madini kufanya kazi kwa bidii kwa ajili ya kuwatumikia watanzania huku wakitanguliza uzalendo.

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa