Home » » ELIMU YA KUZUIA MOTO YATOLEWA KWA WAJUMBE SERIKALI YA KIJIJI CHA RUNGEMBA- IRINGA

ELIMU YA KUZUIA MOTO YATOLEWA KWA WAJUMBE SERIKALI YA KIJIJI CHA RUNGEMBA- IRINGA

Elimu ya kuzuia Moto imetolewa kwa Serikali ya Kijiji Cha Rungemba lengo likiwa ni kutoa tahadhari ya moto hasa katika kipindi hiki cha Kiangazi ambacho kina upepo mkali na wananchi wanasafisha mashamba kwaajili ya kilimo.

Akizungumza Mkuu wa Kitengo Cha Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira Ndugu. Demitrius Kamtoni akiwa ameambatana na Wataalumu kutoka kitengo hicho amesema
Ni muhimu vibali kutolewa na Serikali za vijiji husika kwa  mwananchi anayetaka kusafisha shamba kwa njia ya moto ili tahadhari zote za Moto zichukuliwe

Aidha Ndugu Kamtoni amesema Elimu nyingine iliyotolewa kwa wajumbe hao wa Serikali ya Kijiji cha Rungemba ni:-
-Sheria ya Udhibiti wa Moto
-Taratibu za Uchomaji Moto
-Uhifadhi wa Mazingira
-Utawala Bora wa Maliasili
-Ufugaji wa Nyuki na Vikundi vya Ufugaji Nyuki.

Elimu ya kuzuia moto, Utunzaji wa Hifadhi ya Mazingira na Maliasili itaemdelea kutolewa katika Kata zote za Halmashauri ya Mji Mafinga kwenye ngazi ya Kijiji na Mitaa kupitia Kitengo Cha Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira.

Imeandaliwa na Sima Bingileki
Mkuu wa Kitengo Cha Mawasiliano Serikalini- Mafinga TC

 

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa