Home » » USIMAMIZI WA MIRADI YA MAENDELEO

USIMAMIZI WA MIRADI YA MAENDELEO

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Mafinga Bi. Fidelica Myovella ameendelea na kusimamia Miradi ya Maendeleo kwa kuhakikisha inakamilika kwa Ubora wa fedha zinazotumika na kwa wakati.

Akiwa ameambatana na baadhi ya Wakuu wa Idara akiwepo Afisa Elimu Sekondari Mwalimu Stephen Shemdoe leo tarehe 14/9/2024  Bi. Myovella amesimamia na kutembelea Ujenzi wa bweni la Wasichana katika Shule ya Sekondari JJ Mungai ambapo ujenzi upo hatua  lenta.

Aidha amekagua Ujenzi wa vyumba vitatu  vya madarasa katika Shule ya Msingi Kilimani ambapo maadalizi ya Upauaji yanaendelea.

Akiwa katika zoezi hilo la Usimamizi wa Miradi hiyo amewaagiza Idara husika zinazotekeleza Miradi hiyo kuwa karibu na mafundi ili kubaini changamoto yoyote inapotokea ili itatuliwe kWa haraka na Miradi ikamilike ndani ya muda uliopangwa.

Wakati huo huo Bi Myovella amekagua ujenzi unaoendelea katika Shule ya Msingi Ifingo, ujenzi  wa vyumba viwili vya darasa ambapo ujenzi upo hatua ya kupaua na Ujenzi wa nyumba ya mwalimu 2 in 1 katika Shule ya Sekondari ya Ndolezi ambayo ipo hatua ya lenta.

Aidha amepongeza kwa kasi na ubara wa Miradi inayoendelea.

Imeandaliwa na Sima Bingileki
Mkuu wa Kitengo Cha Mawasiliano Serikalini Mafinga TC


0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa