Home » » TASAF YAMUWEZESHA MNUFAIKA MWENYE UONI HAFIFU KULETA BIDHAA KATIKA MAONESHO YA NANE NANE MBEYA 2024.

TASAF YAMUWEZESHA MNUFAIKA MWENYE UONI HAFIFU KULETA BIDHAA KATIKA MAONESHO YA NANE NANE MBEYA 2024.

Na Sima Bingileki
Afisa Habari Mafinga Tc

“ Kwa kweli tunaishukuru Serikali  ya Awamu ya Sita ya Mama Samia Suluhu Hassan kipitia TASAF tumeweza kushiriki Maonesho haya ya Nane Nane Jijini Mbeya kwani tumeleta majiko ya kupikia ya udogo tuliyoyafinyanga wenyewe,Hatujawahi kuwaza kuwa kuna siku na sisi tutafika Mbeya kwenye Maonesho haya na kuleta bidhaa zetu , Tunaishukuru sana Serikali”

Kauli hiyo imetolewa na Wanufaika wa TASAF kutoka katika Halmashauri ya Mji Mafinga wilaya ya Mufindi Bi Roida Mgwale(40) Mkazi wa Rungemba na Bi Honorina Nyongole(40) Mkazi wa Rungemba Mafinga mwenye Uoni Hafifu na mfinyanzi wa vyungu na majiko ya Udongo.

“Mimi nilikuwa na hali duni sana, kwa sasa nimekuja na majiko ya udongo 12 yangu mwenyewe na ninasomesha watoto, ninafuga na nina kuku 30 na ninakikundi naweza kununua hisa na udongo wa kutengenezea majiko mwenyewe. Nina uoni hafifu lakini TASAF kwa kweli wameweza kubadirisha maisha yangu na familia yangu” Honorina Nyongole Mnufaika

Naye Bi. Roida Ngwale(40) Mmoja
Wa wanufaika wa TASAF na mfinyanzi wa Vyungu na Majiko ya udogo amesema amewezeshwa na TASAF na amekuja na majiko30 pia anafuga kuku wa kienyeji, kusomesha  watoto na kilimo.

Halmashauri ya Mji Mafinga inashiriki maonesho ya Nane Nane Jijini Mbeya katika Viwanja vya John Mwakangale 2024 na kupitia Kitengo cha Maendeleo ya Jamii wanufaika wa TASAF  wawili Bi.Roida Ngwale na Bi.Honorina Nyongole wameweza kushiriki na kuonyesha bidhaa zao.

IMEANDALIWA NA SIMA MARK BINGILEKI
AFISA HABARI MKUU- MAFINGA TC

 

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa