Home » » MKURUGENZI SHULE ZA REALHOPE AKABIDHI KOMPYUTA TATU KWA HALMASHAURI YA MJI MAFINGA

MKURUGENZI SHULE ZA REALHOPE AKABIDHI KOMPYUTA TATU KWA HALMASHAURI YA MJI MAFINGA

“Lengo langu ni kuunga Mkono juhudi zinazofanywa na Serikali hii na naahidi kuendelea kujitolea ili jamii iendelee kunufaika hasa katika Sekta ya Afya na Elimu,  kompyuta hizi 3 (Dell )zitarahisisha uwekaji wa takwimu na utunzaji wa kumbukumbu kidigitali hivyo kupunguza wagonjwa kukaa muda mrefu kusubiri huduma.”

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Shule za Really Hope zilizopo Mji Mafinga Ndugu Dickson Mwipopo alipokuwa akikabidhi kompyuta 3 aina ya Dell zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 5 kwa Mkurugenzi Mji Mafinga Bi , Fidelica Myovella kwaajili ya matumizi ya Sekta ya Afya.
Akipokea compyuta hizo Mkurugenzi Mji Mafinga akiwa ameambatana na baadhi ya Wakuu wa Idara amesema  Msaada huu wa compyuta tatu utarahisisha utunzaji bora wa kumbukumbu na kuweka takwimu Sahihi kwa njia ya kidigitali, hivyo kupunguza kufanya kazi kwenye karatasi( paper work) kwani Serikali inahamasisha matumizi ya mifumo Sahihi iliyowekwa ili kuweka urahisi na huduma kwa haraka.

“ Serikali inathamini sana Wawekezaji ndio maana hata imeanzisha Wizara ya Uwekezaji lengo likiwa ni kuthamini juhudi za Wawekezaji na kuwapa mazingira bora ya kuwekeza bila urasimu, hivyo tunathamini juhudi zako kwani tunafahamu uwekezaji wako katika sekta hii ya Afya unaunga mkono jubudi za  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuboresha huduma za Afya nchini, tunakuahidi kuzitunza kompyuta hizi na kuzitumia kwa lengo kusudiwa.

Akitoa ufafanuzi kuhusu matumizi ya kompyuta hizo 3 zilizotolewa na Mkurugenzi wa Shule za Realhope Ndugu.Dickson Mwipopo, Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mji Mafinga Dkt. Bonaventura Chitopella amesema compyuta hizo zitawekwa Chumba cha Upasuaji na Maabara katika Hospital ya Mji Mafinga na moja itawekwa Zahanati ya Upendo kati Kata ya Upendo

Ndugu Charles Mwaitege Mkuu wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu ametoa neno la shukrani kwa Mkurugenzi wa Realhope kwa Msaada wa Kompyuta 3 na kuahidi matumizi sahihi ya kompyuta hizi na kuleta mabadiliko sehemu zilizokuwa na changamoto ya upungufu wa vifaa hivyo.

Imeandaliwa na
Sima Bingileki
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Mafinga TC

 

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa