Home » » TUWE MAKINI NA TAARIFA TUNAZOZITOA - MKURUGENZI HALMASHAURI YA MJI MAFINGA

TUWE MAKINI NA TAARIFA TUNAZOZITOA - MKURUGENZI HALMASHAURI YA MJI MAFINGA

“Mwaka huu 2024 ni mwaka wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, hivyo tuwe makini na taarifa tunazozitoa ofisini kwetu zisiende kutumika kwenye matumizi yasiyo sahihi na tutoe taarifa sahihi muda utakapo fika kwenye maboresho ya daftari la kudumu la wapiga kura.”
 
Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Mafinga Bi, Fidelica Myovella alipokuwa akizungumza na Watendaji wa Kata, Wakuu wa Idara na vitengo, Wakuu wa Shule na Walimu Wakuu katika ukumbi wa JJ MUNGAI Mjini Mafinga.

Aidha amewataadharisha kutoa taarifa sahihi pale wanapotakiwa kutoa taarifa hizo kwa kibali maalumu ili kuhakikisha taarifa zinazoenda kwenye jamii hasa kipindi cha kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ziwe taarifa Sahihi.

Naye Afisa Mwandikishaji Uboreshaji wa Daftari la kudumu la Wapiga Kura Ndugu, Charles Mwaitege amesema Halmashauri ya Mji Mafinga katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa itakuwaa na Vituo visivyopungua 145 vya Kupigia Kura.
“ Halmashauri ya Mji Mafinga katika Kuboresha Daftari la Kudumu la Wapiga Kura tunaendelea kujipanga na makadirio ni kuwa na wapiga kura 72,939 katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka huu 2024 na vituo  visivyopungua 145 vya kupigia kura”

Halmashauri Ya Mji Mafinga ina Jimbo Moja la Uchaguzi la Mafinga Mjini, lenye Kata 9, Mitaa 30 Vijiji 11 na Vitongoji 50.

Imeandaliwa na
Sima Bingileki
Mkuu wa Kitengo Cha Mawasiliano Serikalini- Mafinga TC

 

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa