Home » » KITUO CHA AFYA UPENDO KUPUNGUZA MSONGAMANO KATIKA HOSPITATALI MJI MAFINGA

KITUO CHA AFYA UPENDO KUPUNGUZA MSONGAMANO KATIKA HOSPITATALI MJI MAFINGA

“ KITUO HIKI CHA AFYA UPENDO KIKIANZA KUTOA HUDUMA KITAPUNGUZA MSONGAMANO KATIKA HOSPITALI YA MJI MAFINGA NA HALI YA WANANCHI KUTEMBEA UMBALI MREFU KUFUATA HUDUMA ZA AFYA.TUNASHAURI KIANZE KUTOA HUDUMA”

Kauli hiyo imetolewa na Wajumbe ambao ni Waheshimiwa Madiwani wa Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya walipofanya ziara kukagua Miradi ya Maendeleo inayotekelezwa chini ya Kamati hiyo. Miradi iliyotembelewa ni ukamilishaji wa Jengo la Maabara katika Kituo cha Afya Upendo na Jengo la Mama na Mtoto katika Zahanati ya Rungemba.

Akisoma taarifa ya Ujenzi wa Maabara katika Kituo cha Afya Upendo Mtendaji wa Kata ya Upendo Bi.Marry Luka amesema ujenzi wa Maabara ulianza tarehe 2/9/2023 baada ya kupokea fedha shilingi Milioni 50 kutoka Serikali Kuu, baadae Halmashauri ya Mji Mafinga kutoka katika Mapato yake ya ndani ikatoa shilingi Milioni 20 ili kukamilisha ujenzi wa Maabara hiyo.

Ameongeza kuwa kazi zinazoendelea ni uwekaji wa Milango, Meza za maabara, Masinki.

Waheshimiwa Madiwani wa Kamati hiyo wamempongeza Mkurugenzi Mji Mafinga Bi. Fidelica Myovella kwa kazi nzuri ya utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo na Ushirikishaji wa Wataalamu, Watendaji wa Kata na kamati za Ujenzi katika Miradi hiyo. Aidha wameagiza ukamilishaji wa Maabara ufanyike haraka ili kituo kianze kutoa huduma kama ambavyo maelekezo ya Serikali yanataka.

Kata ya Upendo katika Halmashauri ya Mji Mafinga  ni moja katika ya Kata Tisa za Mji Mafinga ina jumla ya Mitaa Mitano na wakazi wasiopungua Elfu 25.

Imeandaliwa na
Sima Mark Bingileki
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini- Mafinga TC

 

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa