Home » » TAASISI ZA FEDHA ZAPEWA SOMO

TAASISI ZA FEDHA ZAPEWA SOMO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Mama Bahati Foundation (MBF), Japhet MakauTAASISI za kifedha zinazojihusisha na utoaji wa mikopo kwa wajasiriamali nchini, zimetakiwa kuacha mfumo wa kuwakandamiza wanachama wake kwa riba kubwa, kwa madai kuwa  zinachangia kudumaza  shughuli za kiuchumi na mustakabali wa maisha ya wateja wake.
Rai hiyo ilitolewa mjini hapa hivi karibuni na Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Mama Bahati Foundation (MBF), Japhet Makau, katika mafunzo ya wanachama viongozi wa vikundi vya asasi hiyo.
Alisema taasisi za kifedha zisitegemee zaidi kujiendesha kwa riba za wanachama, kwani hatua hiyo itawafanya wateja kufilisika kwa kushindwa kurejesha mikopo, na kuishia kufilisiwa mali zao na kurejea katika hali ya umasikini.
“Wito wangu kwa asasi za kifedha wanapofanya shughuli zao na wateja wao hao wadogo wadogo lengo kuu linapaswa liwe ni kuwasaidia masikini kwa kuwatoa katika hali duni na kuwawezesha kuwa katika hali nzuri, tusiweke suala la faida mbele, kwani ukiweka lengo la faida utamdidimiza masikini na kuwa masikini zaidi,” alisema Makau.
Alisema mfuko huo hadi sasa umeshatoa zaidi ya sh bilioni 5 kwa wanawake wa Manispaa ya Iringa, Iringa Vijijini na Wilaya ya Kilolo na kusema kuwa lengo la mfuko huo si kutengeneza faida bali ni kuwawezesha wafanyabiashara wenye mitaji midogo.
Mwanzilishi wa mfuko huo, Askofu Mkuu mstaafu, Donald Mtetemela, alisema upo umuhimu wa kuendeleza mpango huo kwa kinamama, ili kuwainua kiuchumi, baada ya mama aliyemsaidia sh 10,000 kuendeleza biashara yake kuonyesha uaminifu, hatua iliyofanya kumuongeza kiwango hadi kufikia sh 50,000.
Hata hivyo, mama huyo, Diana Mbembela aliyekuwa akitembeza ndizi mitaani, hivi sasa ni marehemu.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa