Home » » LEMA:AIBU TANZANIA KUWA OMBAOMBA

LEMA:AIBU TANZANIA KUWA OMBAOMBA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
MBUNGE wa Arusha Mjini, Godbless Lema, amesema Tanzania inatia aibu kwa kugeuka ombamba huku ikiwa na rasilimali nyingi ambazo zinawafaidisha wachache wasiona uchungu na nchi.
Lema, alitoa kauli hiyo hayo juzi alipowahutubia wakazi wa Kata ya Miyomboni-Kitanzini  katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa Mnada (Well Fair) katika Manispaa ya Iringa.
Alisema watu wanaoiba rasilimali za nchini wanalindwa kama dhahabu huku masikini wakibambikiziwa kesi za ajabu ajabu.
“Ndugu zangu, tunapopambana na CCM, tunapambana na wezi, majambazi, mafisadi, wahuni na mafilauni. Unapokuwa na chama kinachouza ndovu, madini, misitu, na ardhi, uhusiano wao na shetani ni wa karibu.
“Unapokuwa na chama kinachotoa sukari kiwandani kwa sh 1,000 na kutoza kodi hadi kufikia 2,000 au ukiwa na chama ambacho saruji kiwandani inatengenezwa kwa sh 4,000 na kutoza kodi hadi kufikia sh 15,000 ni chama cha mauaji,” alisema Lema.
Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa, alisema ikiwa nchi yenye rasilimali nyingi kama Tanzania inategemea asilimia 40 ya bajeti znima kutoka kwa wahisani na wafadhili mbalimbali, nchi haina viongozi wenye uwezo wa kufiki jinsi ya kujitegemea.
Alisema cha kushangaza kuna wabunge ambao wapo madarakani kwa miaka mingi, lakini majimbo yao hayana maendeleo kwa muda mrefu. lakini kazi yao ni kuunga mkono bajeti hewa.
“Mipango yote inaandaliwa kwa ajili ya matajiri na makampuni makubwa yanayokweta kulipa kodi pamoja na kuiba rasilimali za umma au kuwaibia Watanzania” alisema.
Alisema inapoonekana mmoja anaonewa, jamii inapaswa kupiga kelele kwa kuwa kuonewa kwa mtu mmoja ni kuonewa kwa jamii nzima.
 “Akionewa machinga, nesi hapaswi kukaa kimya, akionewa mwalimu machinga hapaswi kukaa kimya. Watu wote tunategemeana kwa kazi tunazozifanya” alisema.
 Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa