Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
HATIMAYE kinyang’anyiro cha kumsaka Redd’s Miss Iringa kinatarajia
kufanyika Juni 20, baada ya aliyekuwa Mratibu wa kwanza, Mohamed
Mcholeka kutoweka katika mazingira ya kutatanisha na kushindwa
kufanyika Juni 6 kama lilivyokuwa imepangwa.
Hivi karibuni, Tanzania Daima iliripoti kutoweka kwa
Mcholeka katika mazingira ya kutatanisha, huku wadau wa urembo
wakiwataka waratibu wa Miss Tanzania, Kampuni ya Lino Agency chini ya
Hashim Lundenga ‘Uncle’ kumchukulia hatua na kuliokoa shindano hilo.
Lino Agency baaada ya kugundua hilo, wamempa kibali cha kuandaa
shindano hilo ambalo lilikuwa linasubiriwa kwa hamu kubwa na wadau wa
tasnia ya urembo, Kampuni ya Chakudika Entertainment chini ya uongozi
wake, Victor Chakudika, ambaye ni meneja wa kituo cha redio cha Nuru Fm
cha mjini hapa.
Akizungumza na Tanzania Daima ofisini kwake jana, Chakudika
alisema uamuzi wa kuchukua jukumu hilo kwa sasa, umelenga kutopoteza
vipaji vya mabinti waliokuwa tayari kushiriki shindano hilo na kuondoa
aibu ya Mkoa wa Iringa kutopeleka mwakilishi katika shindano la Redd’s
Miss Nyanda za Juu, ambako wamekuwa wakishiriki kila mwaka.
Alisema kuwa shindano la Redd’s Miss Iringa limekuwa chachu ya ajira
kwa mabinti wengi mkoani hapa, kwa kuweza kutangaza vipaji vya
washiriki wanaojitokeza kushiriki kila mwaka.
Chakudika alisema shindano hilo linatarajiwa kuwa la kisasa kutokana
na maandalizi yake kuendelea vema na kuwataka wadau wa tasnia ya
urembo, kujitokeza kwa wingi katika Ukumbi wa St. Dominic
litakapofanyika shindano hilo.
Aliongeza kuwa hadi sasa warembo 12 wamejitokeza kushiriki shindano
hilo na wanaendelea na mazoezi katika Ukumbi wa Hoteli ya Gentle Hill
mjini hapa na msanii Mo Music anayetamba na wimbo ‘Basi Nenda’
anatarajia kutoa burudani kali katika shindano hilo, sambamba na
wasanii wengine chupukizi wa mjini Iringa, vikundi vya sanaa na ‘Wakali
wa Kudance’ wa mjini Iringa.
Mbali na Redd’s, wadhamini wengine ni Nuru Fm, kampuni mpya ya mabasi ya Sutco High Class na Gentle Hills.
Chanzo;Tanzania Daima
0 comments:
Post a Comment