Home » » WAJASIRIAMALI WA NYUKI WAPEWA VIFAA KAZI

WAJASIRIAMALI WA NYUKI WAPEWA VIFAA KAZI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Wajasiriamali wa nyuki wapewa vifaa kaziMFUKO wa Hifadhi ya Misitu Tanzania (TaFF) kwa kushirikiana na Mtandao wa Jamii wa Usimamizi wa Misitu Kanda ya Kitapilimwa (MJUMIKK) umewakabidhi wajasiriamali mashine sita za kukamua asali na mizinga 20.

Vifaa kazi hivyo vilipokelewa na vikundi vya ujasiriamali vinavyorina asali kata za Kitapilimwa na Kiwele, Ismani mkoani Iringa.
Akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano iliyofanyika katika Kijiji cha Kinywang’anga hivi karibuni, Katibu wa mtandano wa MJUMIKK, Samson Fuko, alisema lengo ni kuleta ufanisi wa kulinda, kutunza na kutumia kwa njia endelevu rasilimali za misitu na kuongeza kipato cha mjasiriamali.
Alisema mashine hizo zitakuwa shamba darasa la ufugaji wa nyuki na upandaji miti utakaotoa mafunzo ya vitendo kwa wanachama wake na elimu kwa jamii juu ya uhifadhi wa mazingira.
Fuko alisema mtandao huo umefanikiwa kuongeza idadi ya wanachama kutoka 50 waliokuwepo awali hadi 200 waliopo sasa ambao wanajihusisha na ufugaji wa nyuki unaotekelezwa katika vijiji sita kati ya 11 vya Ismani.
Alivitaja vikundi vilivyofaidika na msaada huo kuwa ni Kinywang’anga, Faraja Group, Twiga Group, Mshikamano, Jitegemee na Umoja, vilivyopatiwa mizinga, mashine, zana za kukamulia asali na mavazi maalumu ya kurinia asali vyenye thamani ya sh milioni 4.5.
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Iringa, Jesca Msambatavangu, aliyeshuhudia makabidhiano hayo, aliwaasa wazazi na walezi kuwahamasisha vijana wao wajiunge kwenye shughuli za maendeleo.
Chanzo:Tanzania Daima 

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa