Home » » FIFA, TFF KUJENGA UWANJA IRINGA

FIFA, TFF KUJENGA UWANJA IRINGA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

CHAMA cha Soka Mkoa wa Iringa (Irefa), kwa kushirikiana Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), na Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA), wanatarajiwa kujenga uwanja wa kisasa katika eneo la Kitwiru mkoani hapa.
Hayo yalibainishwa juzi, wakati aliyekuwa Katibu Mkuu wa Irefa, Eliud Mvela ‘Wamahanji’ ambaye kwa sasa ni Mkurugenzi Msaidizi wa Sheria na Uanachama wa TFF, wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa hoteli ya Embalasasa, kwa lengo la kuwaaga na kutoa shukrani kwa ushirikiano kipindi cha uongozi wake.
Alisema, wanatarajia kujenga Uwanja huo, ambao utakuwa chini ya Baraza la Wadhamini, hivyo kuruhusu michezo mikubwa kufanyika na kuongeza hamasa kwa vijana kujiajiri kupitia sekta ya michezo.
“Moja ya mafanikio ambayo nitayaacha ni jitihada za kuanza makakati wa ujenzi wa uwanja wa kisasa wa nyasi bandia katika Manispaa ya Iringa, utakaojengwa eneo la Kitwiru chini ya ufadhili wa FIFA na TFF na kuwa, jitihada za ujenzi zinaendelea kufanyika na Manispaa ya Iringa tayari imetoa eneo,” alisema Wamahanji.
Wamahanji alisema, mchakato wa kuujenga uwanja huo umeanza na barua ya kukubaliwa imeshatoka na utakuwa moja ya viwanja vitano bora Tanzania, hivyo kusaidia kukuza soka la Mkoa wa Iringa.
Aliongeza kuwa, katika uongozi wake mengi amefanya, ikiwemo kuacha timu mbili zinazoshiriki ligi daraja la kwanza na kuondoa migogoro ndani ya chama ambayo ilikuwepo hapo kabla.
Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa