Home » » Wasomi vyuo vikuu watakiwa kujiunga na VETA

Wasomi vyuo vikuu watakiwa kujiunga na VETA


WASOMII wa vyuo vikuu kote nchini wameshauriwa kujiunga na vyuo vya mafunzo ya ufundi Stadi "VETA", ili kujiongezea ujuzi na maarifa ya kufanya kazi, kwa lengo la kujiajiri wenyewe katika sekta binafsi, hatua ambayo itapunguza utegemezi wa ajira serikalini.
Wito huo  umetolewa na mkuu wa Mkoa wa Iringa Dr. Christin Ishengoma, wakati akifungua mkutano wa wakuu wa vyuo vya ufundi VETA,  vilivyopo katika mikoa ya Kusini, mkutano uliolenga kupeana mikakati juu ya utaratibu wa uendeshaji wa vyuo katika mfumo mpya wa Compitance Base Assesment (CBI) - mkutano uliyofanyika katika chuo cha ufundi cha Donbosco cha Manispaa ya Iringa.
Dr. Ishengoma amesema pia wazazio na walezi wanapaswa kuachana na dhana potofu ya kuwa vyuo vya Veta vipo kwa ajili ya wasio na elimu pekee, huku akiitaka kuwapeleka vijana wao katika vyuo hivyo vya ufundi vilivyosajiliwa, na kuwataka wakuu wa vyuo kuajiri walimu wenye sifa.
 
Mkurugenzi wa vyuo vya Veta Nyanda za juu kusini Monica Mbelle amesema Kanda ya kusini ina jumla ya vyuo vya veta 74, huku mkoa wa Iringa ukiwa na vyuo 29, mkoa wa Njombe vyuo 23 Ruvuma pamoja na mkoa wa Ruvuma 22.
 
Bi. Mbelle amesema katika msimu wa mwaka 2013/ 14 Veta inampango wa kujenga vyuo vya Veta katika wilaya ya Ludewa, Chuo cha Wilaya ya Namtumbo pamoja na ujenzi wa chuo cha Mkoa wa Njombe.


0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa