Home » » Utapiamlo waitesa Iringa

Utapiamlo waitesa Iringa


LICHA ya mkoa wa Iringa kuwa ni kati ya mikoa sita inayotegemewa kwa chakula kitaifa, bado mkoa huo unakabiliwa na tatizo la ugonjwa wa Utapiamlo, ugonjwa unaotokana na mlo duni, jambo ambalo linadhihilisha kutokuwepo kwa elimu ya lishe kamili.
Hayo yamezungumzwa na mkuu wa mkoa huo wa Iringa Dr. Christine Ishengoma, wakati wa uzinduzi wa ghara la mbolea ya Yara, eneo la Ipogolo mjini Iringa, ambapo mkuu huyo amesema tatizo  la lutapiamlo linawaathiri zaidi wajawazito, watoto pamoja na wazee.
Dk. Ishengoma amesema mkoa huo wa Iringa umeshika nafasi ya tatu kati ya mikoa inayokabiliwa na ugonjwa wa Utapiamlo, nafasi ya kwanza ikishikiliwa na mkoa wa Dodoma mkoa ambao unakabiliwa na changamoto ya uhaba wa mvua.
Aidha mkuu huyo wa mkoa amesema ugonjwa wa utapiamlo kwa watoto walio na umri chini ya miaka mitano mkoa wa Iringa unashika nafasi ya tatu kitaifa kwa asilimia 52, na kuwa hiyo ni aibu kubwa kwa mkoa kutokana na Iringa kuwa na vyakula vya kutosha.
Dk. Ishengoma amesema kitaifa, mkoa wa Dodoma unaongoza kwa kuwa na Utapiamlo mkali kwa asilimia 56, huku ukifuatiwa na mkoa wa Lindi wenye asilimia 54, huku akiwaasa mawakala kuacha tabia ya kutochezea vocha za ruzuku ya pembejeo za kilimo kwa madai kuwa hali hiyo inawakwamisha wakulima.
Hata hivyo ofisa biashara wa kampuni ya Yara Hilary Pato amesema lengo la kampuni ya yara kusogeza huduma mkoani Iringa ni kuwasaidia wakulima kufikia malengo ya kilimo chenye tija kwa kupata pembejeo kwa wakati unaofaa.



0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa