Home » » MAMIA WAJITOKEZA KUMZIKA ALIYEKUWA KATIBU WA CCM MKOA WA IRINGA LEO

MAMIA WAJITOKEZA KUMZIKA ALIYEKUWA KATIBU WA CCM MKOA WA IRINGA LEO

 Vijana  wa  UVCCM mkoa  wa Iringa na Mbeya  wakiwa  wamelibeba  jeneza  lenye  mwili wa aliyekuwa katibu wa CCM mkoa wa Iringa Emanuel Mteming'ombe leo  wakati  wa kuelekea  kanisani kwa ibada kabla ya mazishi yake  yaliyofanyika kijijini Kwake Rujewa Mbarali mkoani Mbeya
Naibu katibu mkuu wa CCM Bara Bw Mwigulu Nchemba wa pili kulia akiwa na mwenyekiti wa CCM mkoa  wa Iringa Jesca Msambatavangu kulia na viongozi  wengine nyumbani kwa marehemu Mteming'ombe Rujewa Mbarali
Mkuu  wa mkoa  wa Mbeya  Abas Kandoro wa pili  kushoto akiwa na mkuu wa mkoa wa Iringa Dr Christine Ishengoma katikati
Familia ya marehemu na ndugu mbali mbali  wakiwa kanisani kanisa la RC Rujewa  leo
Waombolezaji  wakiwa ibadani  leo
Naibu katibu mkuu CCM Bara Bw Mgulu Nchemba akiongoza  waombolezaji  kutoa  heshima zake za mwisho kwa aliyekuwa katibu wa CCM mkoa wa Iringa Emanuel Mteming'ombe leo katika kanisa la RC Rujewa Mbarali mkoani Mbeya
Mkuu  wa mkoa  wa Iringa Dr Christine Ishengoma akitoa  heshima zake
Mwenyekiti wa CCM mkoa  wa Iringa Jesca Msambatavangu  akiaga mwili  huo
Waombolezaji  wakikimbia mvua  kubwa iliyonyesha kwa dakika kama 10  hivi mara baada ya  mwili kufika makaburini
Mwenyekiti  wa CCM mkoa  wa Iringa Jesca Msambatavangu  akisoma historia ya marehemu Mteming'ombe huku naibu katibu mkuu  CCM Bara Bw Nchemba akionyesha kufuta machozi
Mjane  wa Mteming'ombe akiweka maua
Mzee Mteming'ombe akiweka shada la maua
Naibu katibu mkuu CCM Bara  Mgulu Nchemba  akiongoza  waombolezaji kuweka shaba la maua  katika kaburi la aliyekuwa katibu wa CCM mkoa wa Iringa marehemu Emanuel Mteming'ombe leo katika makaburi ya RC Rujewa Mbarali Mbeya
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa Jesca Msambatavangu  akiweka shada la maua
mkuu  wa  mkoa wa Iringa Dr Ishengoma  akiweka  shada la maua
Mkuu  wa mkoa  wa Mbeya Abas  Kandoro akiweka shada la maua
Kanali Mjengwa akisalimiana na naibu katibu mkuu CCM Bara Mgulu Nchemba  leo nje ya kanisa la RC Rujewa baada ya  kukutana kwa shughuli za mazishi ya aliyekuwa katibu wa CCM mkoa  wa Iringa Emanuel Mteming'ombe Na Francis Godwin Blog

MWENYEKITI wa  Chama cha  mapinduzi (CCM) Taifa  Dr  Jakaya  Mrisho  Kikwete  ametuma  salam  za rambirambi kwa  uongozi  wa  CCM mkoa  wa  Iringa na  familia ya aliyekuwa  katibu  wa CCM mkoa  wa  Iringa Emanuel Mteming'ombe aliyefariki  dunia juzi na kuzikwa  leo katika mji  wa  Rujewa Mbarali  mkoani Mbeya.

Salam  hizo  za Rais Dr  Kikwete  zilitolewa  jana   wakati  wa mazishi  ya Mteming'ombe  na naibu  katibu mkuu  CCM Bara  Bw Mwinhulu Nchemba  ambae alikiwakilisha  chama taifa  katika mazishi hayo .

Alisema  kuwa Rais Dr  Kikwete  ambae  yupo  nchini Marekani kwa ziara  za  kiofisi amepokea  kwa masikitiko makubwa  taarifa  ya  kifo  cha katibu  huyo na kuwa alitamani  sana  kuweza kufika Rujewa mkoani Mbeya  kwa ajili ya  kushirikia mazishi  hayo ila ameshindwa .

" Nitoe  salama za aina  tatu  salama ya kwanza  kutoka kwa mheshimiwa Rais Dr  Kikwete akiwa  mwenyekiti  wetu wa Chama taifa  amepokea kwa masikitiko makubwa  taarifa  hii ya kifo  na wakati anapata  taarifa  hii tayari  alikuwa katika ndege  kuelekea  nchini Marekani .....kama  tunavyojua Rais  wetu  ni mwepesi  kufika katika misiba ila ameshindwa na  kuniagiza  mimi  kutoa  salam zake kwa niaba yake"
Hata  hivyo  alisema  kuwa  salama  za pili ni  kutoka kwa katibu mkuu wa CCM Taifa  ambapo amepokea kwa masikitiko makubwa  zaidi  kutokana na kifo  hicho  kutokana na katibu  huyo marehemu Mteming'ombe  enzi  za uhai  wake  alikuwa msaada mkubwa  sana kwa chama  kutokana na kuwa mwepesi  zaidi.

Alisema kuwa  wao kama  chama   wataendelea  kuwa karibu na familia ya marehemu ikiwa ni pamoja na kuitunza  familia  hiyo.

Kwa  upande  wake  mkuu wa mkoa  wa  Iringa Dr Christine Ishengoma akitoa  salama za  serikali mkoa  wa Iringa  kufuatia  kifo  hicho alisema  kuwa katika  kipindi  hiki cha maombolezo  na  baada ya maombolezo  viongozi wa chama na  serikali mkoa  wa Iringa  hawana budi kuendelea  kufanya kazi kwa  kushirikiana  zaidi kama njia ya  kumuenzi Mteming'ombe.

Huku  mkuu  wa  mkoa  wa Mbeya Abas  Kandoro akisisitiza viongozi  wa umma na chama  kujenga  utamaduni  wa kushirikiana na kuacha  tabia ya kujitenga na jamii.

Wakati  huo  huo waombolezaji  waliofulika makaburini hapo walionyesha  kushindwa  kujizuia kushangilia kwa  furaha  kubwa wakati mwenyekiti  wa CCM mkoa  wa Iringa Jesca  Msambatavangu  akisoma mchango wa  waziri mkuu aliyejiuzulu Edward Lowasa mchango  wa Tsh milioni 1  alioutuma kwa uongozi  wa CCM mkoa wa Iringa kwa ajili ya shughuli  za mazishi  ya  Kiongozi  huyo.
Katika  tukio  jingine  vijana  wanaosadikika kuwa na wafuasi  wa Chadema  wakiwa na sare za chama hicho wamejikuta  wakichezea  kichapo  kutoka kwa vijana  wa UVCCM baada ya kuwavamia  vijana hao katika kanteni ya  polisi Rujewa ambako  walikuwa  wakijipumzisha kwa uchovu .
Imedaiwa  kuwa  vijana wapatao wanne  walifika eneo hilo na kuanzisha  vurugu hali  iliyopelekea vijana wa UVCCM kutoka mkoa  wa Iringa na Mbeya  kuwafunza adabu na polisi  kuwakamata  vijana  hao wa Chadema na kuwatupa mahabusu.
Mwenyekiti wa UVCCM mkoa  wa Iringa Tumain Msowoya  alisema amezipata habari  hizo japo alisema kuwa hakuna majeraha makubwa yaliyowapata  vijana wa CCM mbali ya wavamizi hao kuwa shambulia kwa chupa .



AWALI AKISOMA WASIFU WA MAREHEMU EMMANUEL MTEMING’OMBE ,MWENYEKITI  WA CCM MKOA WA IRINGA JESCA  MSAMBATAVANGU ALISEMA

Marehemu Emmanuel Mteming’ombe alizaliwa tarehe 25/ 06/ 1956 katika kijiji cha Rujewa, Wilaya ya Mbarali, Mkoa wa Mbeya.

2.     ELIMU NA MAFUNZO.

Marehemu Emmanuel Mteming’ombe alipata elimu yake ya msingi katika shule ya msingi Chimala, Mbeya kati ya mwaka 1972 – 1978. Baada ya kumaliza darasa la saba, marehemu alijiunga na masoma ya sekondari katika shule ya sekondari ya wavulana Songea kuanzia mwaka 1979 – 1982.
Kati ya mwaka 1986 -1989 marehemu alijiunga na Chuo cha Uganga Songea akisomea kozi ya Utabibu.

3.     UTUMISHI WA SERIKALI.

Mwaka 1991, marehemu aliajiriwa serikalini kwa cheo cha Medical Assistant (Tabibu), kazi aliyofanya kwa miaka mnne hadi mwaka 1994 alipoamua kuacha kazi na kufungua Duka la Dawa na Zahanati yake binafsi.

4.     UTUMISHI KATIKA CHAMA CHA MAPINDUZI.

Nyota njema huonekana asubuhi. Marehemu Emmanuel Mteming’ombe akiwa Chuo cha Utabibu Songea kati ya mwaka 1986 – 1989 alichaguliwa kuwa mwenyekiti wa Umoja wa vijana Tawi kwa muda wote aliokuwa Chuoni hapo.

Mara baada ya kumaliza masomo yake ya Utabibu alipata tena nafasi ya kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa UVCCM wa kata ya Rujewa, Mbarali kuanzia mwaka 1990 – 1994. Kutokana na uhodari aliouonesha, marehemu mwaka 1994 alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa kijiji cha Rujewa hadi mwaka 1999.

Mwaka 1998, Marehemu Emmanuel Mteming’ombe alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Mbeya, nafasi aliyoshika hadi mwaka 2003. Katika uchaguzi Mkuu wa Serikali wa mwaka 2000,Marehemu alichaguliwa kuwa Diwani wa kata ya Rujewa, nafasi aliyoshika hadi octoba, mwaka 2005.

Kutokana na uwezo wake mkubwa wa Uongozi aliouonesha katika nafasi mbalimbali za uongozi, Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM iliyokutana tarehe  26 – 27/ 03/ 2003 ilimteua kuwa Kaimu Katibu wa CCM wa Wilaya na kupangiwa kwenda kufanya kazi katika wilaya ya Kyela. Baada ya kuonekana anamudu nafasi ya Katibu  wa CCM wa Wilaya, Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa iliyokutana tarehe 19 -20/ 03 2004 ilimthibitisha kuwa Katibu wa CCM wa Wilaya.

Marehemu Emmanuel Mteming’ombe, akiwa Katibu wa CCM wa Wilaya alifanya kazi katika Wilaya za Kyela, Ireje, Mbozi ambako alionyesha uwezo mkubwa wa Uongozi na kuwa tegemeo la Chama Cha Mapinduzi.

Marehemu Emmanuel Mteming’ombe aliteuliwa kuwa Kaimu Katibu Wa CCM wa Mkoa wa Mbeya, kuanzia tarehe 29/ 01/ 2008 na baadaye kuwa Katibu wa Mkoa na kumpangia kwenda katika Mkoa wa Ruvuma ambako alifanya kazi hadi tarehe 28/ 05/ 2012 alipohamishiwa Mkoa wa Iringa.
5.     UGONJWA.

Marehemu Emmanuel Mteming’ombe alianza kuumwa tarehe 02/ 12/ 2013 akieleza kuwa baada ya kuonana na Daktari iligundulika kwamba anasumbuliwa na homa ya Matumbo (Typhoid), Athma na Figo yake ya upande wa kushoto ikaonekana kuwa ina matatizo na kupewa dawa ambapo alirejea nyumbani kwake na kuendelea kutumia.

Ilipofika tarehe 17/ 12/ 2013 usiku, Marehemu alizidiwa na kupelekwa Hospitali Kuu ya Mkoa wa Iringa ambapo madaktari walijitahidi kumhudumia, lakini ilipofika saa 8 usiku wa tarehe 19/ 12/ 2012 alifariki Dunia.
Marehemu ameacha Mjane na Watoto Watatu.
Bwana alitoa na Bwana ametwaa Jina la Bwana Lihimidiwe
Amen.

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa