Home » » Rais Kikwete kuwa mgeni rasmi kwenye kilele cha maadhimisho ya Mwenge wa Uhuru

Rais Kikwete kuwa mgeni rasmi kwenye kilele cha maadhimisho ya Mwenge wa Uhuru

Ikiwa leo ndio mapokezi rasmi ya Mwenge wa Uhuru kitaifa manispaa ya Iringa ,viongozi mbalimbali wamejitokeza kuupokea  mwenge huo huku kesho ikiwa ndo kilele cha Maadhimisho ya mwenge  huku mgeni rasmi akiwa ni rais wa Tanzania DK.JAKAYA MRISHO KIKWETE

Mwenge huo wa uhuru    umepokelewa leo  na mkuu wa wilaya ya kilolo GERALD GUNINITA na kumkabidhi  mkuu wa wilaya ya iringa mjini RETISIA WARIOBA na kuendelea  kuzindua miradi mbalimbali  ikiwemo kituo cha michezo kwa vijana chini ya shirika la IDYDC ili kuendeleza michezo kwa vijana.

Akisoma hutuba kwa mgeni rasmi meneja wa kituo hicho  cha michezo LIGE MASANJA amesema kuwa lengo la kuanzisha kituo hicho cha vijana ni kuona vijana wanapata maendeleo kupitia michezo na elimu

0 comments:

 
Powered by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa