KUKITHIRI kwa
wimbi la uvamizi wa majengo ya taasisi za kifedha nchini, kumezitia shaka benki
za wananchi waishio vijijini - Vicoba, na hivyo kuomba msaada kwa serikali
kuweka ulinzi madhubuti kwa benki hizo ikiwemo kujengwa kwa vituo vya polisi
kila kata.
Wakizungumzia hofu yao ya fedha zao katika
uzinduzi wa Vicoba vya kikundi cha Uamsho na Ulete vya Iringa vijijini,
wanachama hao wamesema fedha zao zipo mashakani kwa kutokana na matukio ya
uvamizi wa benki nchini kukithiri.
Benitho Kimuli mwanakikundi wa Muwimbi Vicoba,
amesema matukio ya ujambazi wa kuvamia benki ni tishio kubwa kwao, kwa madai
kuwa baadhi ya vikundi vingine havina akaunti katika benki na hivyo hulazimika
kuweka fedha zao katika nyumba za viongozi wao.
Diwani wa kata hiyo ya Lumuli Charles Lutego
amesema kuna haja kwa serikali kujipanga zaidi ili kuhakiki ulinzi kwa benki za
wananchi wa vijijini ambazo sasa zimekuwa nyingi lakini hazipo salama kwa
kukosekana kwa vituo vya polisi vya Kata.
Aidha ofisi ya mbunge wa jimbo la Kalenga Dr.
Willium Mgimwa kupitia mwakirishi wake Johakim Mgimwa imetoa ahadi ya
kuviwezesha vikundi hivyo viwili jumla ya shilingi Milioni 5 na laki 5, huku
mwakirishi huyo akiwaasa wanavikundi hao kuwa wabunifu katika kukuza uchumi
wao, na kujitolea kuchangia mahitaji muhimu ya kijamii.
Hata hivyo
mratibu wa Vicoba mkoani Iringa Tisiana Kikoti amewataka wanachama hao kuwa
waaminifu kwa kukopa kwa nidhamu na kurejesha madeni kwa wakati, ili kutoa
nafasi ya wanachama wengine kupatiwa mikopo hiyo.
0 comments:
Post a Comment