Home » » 503 wana maambukizi ya ukimwi Iringa

503 wana maambukizi ya ukimwi Iringa

MIONGONI mwa watu 5,631 mkoani hapa waliopima afya zao katika kipindi cha Julai hadi Septemba mwaka huu, watu 503 wamebainika kuwa na maambukizi ya virusi vya ukimwi (VVU).
Akizungumza katika kikao cha utekelezaji wa shughuli za ukimwi zilizotekelezwa na Kamati ya Kudhibiti Ukimwi mbele ya baraza la madiwani kwa kipindi cha robo ya kwanza ya Julai na Septemba, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Naibu Meya Gervas Ndaki, alisema kati ya waliojitokeza kupima na kupata ushauri nasaha, wanaume walikuwa 2,712 na wanawake 2,919.
Ndaki alisema kati ya watu 503 waliopima kwa hiari na kukutwa na maambukizi, 188 ni wanaume na wanawake ni 315.
Alisema huduma ya kuzuia maambukizi ya vvu/ukimwi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto, wajawazito 1,009 walijitokeza na kupata ushauri wa nasaha na kati yao, 104 walikutwa na maambukizi.
Ndaki alisema mapambano ya ukimwi yanaambatana  na huduma za tiba sahihi ya magonjwa ya ngono na jumla ya watu 564, wanaume 178 na wanawake 386, walipata tiba sahihi ya magonjwa ya ngono.
Chanzo: Tanzania Daima

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa