Home » » Kilolo hatarini kukosa mitihani darasa la VII

Kilolo hatarini kukosa mitihani darasa la VII

BAADHI ya wanafunzi wa darasa la saba wakiwemo watoto yatima wa Shule ya Msingi Kimala, kata ya Kimala wilaya ya Kilolo, mkoani Iringa, huenda wasifanye mitihani yao mwisho kutokana na kukosa michango ya sh 47,000 ambayo wanadaiwa shuleni hapo.
Baadhi ya wanafunzi hao wameliambia gazeti hili kuwa uwezekano wa kutokufanya mitihani upo kutokana kwani hivi sasa hawaruhusiwi kuingia madarasani na madala yake hufanyishwa kazi za nje.
Wanafunzi waliozungumza kwa sharti la kutotaja majina yao, walisema kuwa wamekuwa wakifanyishwa kazi na uongozi wa shule badala ya kusoma kwa sababu hawajalipa michango.
Walifafanua kuwa walizuiliwa kufanya mitihani ya kanda jambo ambalo wananchi walilipigia kelele na kulazimishwa kufanyishwa mitihani saba kwa siku mbili.
Wakizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti, wananchi wa kijiji hicho walisema mwalimu mkuu wa shule hiyo amekuwa mbabe kutaka kila anachokitaka kifanyike pasipo makubaliano na wazazi au kamati ya shule.
Boniface Kasuga ambaye pia ni mjumbe wa kamati ya shule hiyo alieleza kushangazwa na michango hiyo kuwa ni mipango ya watu binafsi.
“Hii michango ni ya uonezi. Mchango wa darasa la saba unakujaje kwa kila mwanafunzi kutozwa sh 47,000?
“Kuna watu wachache ambao wanapanga michango hiyo kama ulaji kwao,” alisema Kasuga.
Mweyekiti wa kamati ya shule hiyo Telaki Ndenga amethibitisha kuwepo kwa michango hiyo na kwamba kamati ya shule haijawahi kushirikishwa juu ya michango hiyo.
Mitihani ya darasa la saba inatarajiwa kuanza Septemba 12, mwaka huu.
Chanzo: Tanzania Daima

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa