Home » » NAIBU MEYA WA MANISPAA YA IRINGA AJIUZULU ,KUPISHA UCHAGUZI MPYA . NAIBU MEYA WA MKOA WA IRINGA APATIKANA

NAIBU MEYA WA MANISPAA YA IRINGA AJIUZULU ,KUPISHA UCHAGUZI MPYA . NAIBU MEYA WA MKOA WA IRINGA APATIKANA

 Aliyekuwa naibu  meya  wa manispaa ya  Iringa G. Ndaki akiomba  kura  kwa  wajumbe kabla ya kujiuzulu
Katibu  wa Chadema wilaya ya Iringa mjini Suzana Mgonakulima na diwani wa kata ya Mvijeni Frank Nyalusi wakifuatilia  zoezi zima la uchaguzi ,Mgonakulima ni diwani wa  viti maalum pia 


 Leo umefanyika uchaguzi wa Naibu Meya katika manispaa ya Iringaambapo ushindi katika uchaguzi huu amekuwa ni GEREVAS NDAKI ambaye alikuwa akishikilia nafasi hiyo toka awali.
 
Uchaguzi huo umefanyika katika kikao cha baraza la madiwani wa manispaa ya iringa  ambapo umeambatana na kamati mbalimbali za baraza hilo ikiwemo kamati ya afya, mazingira fedha na nidhamu.
 
Katika uchaguzi huo ni mugombea mmoja tu ambaye aliwania nafasi hiyo kupitia chama cha mapinduzi ccm na wajume 23 ndio walishiriki katika uchaguzi huo na kura moja iliharibika.
 
Kwa upande wake naibu meya aliyechaguliwa amewashukuru wote waliomchagua na kusema kwa hata hiyo kura moja ambayo haijamchagua anaishukuru pia kwani inatokana na na mhusika kutoridhika na kazi ya ke hivyo bado anaowajibu wa kujipanga upya ili aweze kumfanya mtu huyo akubaliana na uwajibikaji wake.


KWA HISANI YA FRANCIS GODWIN NA JIACHIE BLOG

0 comments:

 
Powered by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa