Home » » IRINGA WAADHIMISHA SIKU YA MASHUJAA

IRINGA WAADHIMISHA SIKU YA MASHUJAA



 Leo ni siku ya maadhimisho ya mashujaa  nchini Tanzania na kitaifa yamefanyika katika mkoa wa kagera,ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Mh. RAIS WA JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, JAKAYA KIKWETE.

Katika mkoa wa Iringa maadhimisho hayo yamefanyika katika viwanja vya bustani ya manispaa ya iringa na mgeni rasmi katika maadhimisho hayo alikuwa mkuu wa wilaya ya kilolo GERALD GUNINITA badala ya mkuu wa mkoa wa Iringa CHRISTINE ISHENGOMA.

Akizungumza katika maadhimisho hayo mkuu wa wilaya huyo amesema kuwa wanaadhimisha siku hii ya leo kwa sababu ya kuwakumbuka mashujaa ambao walipigana uhuru wa taifa letu.

Guninita amesema pia dhumuni la kuwa kumbuka mashujaa hao ni kwa sababu walikuwa wakipambana dhidi ya Nduli Idiamini, ambaye alichokoza Taifa letu mwaka 1978.

Aidha ameongeza kwa kusema kuwa wakazi wa iringa na watanzania kwa ujumla wanapaswa kukumbuka kuwa mashujaa hao walikufa wakati wakipigania amani na uhuru wa taifa letu hivyo ni muhimu kuwaenzi ili kudumisha amani yetu kwa faida ya kizazi cha sasa na cha baadaye.

CHANZO: JIACHIE BLOG

0 comments:

 
Powered by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa