Wapenzi wa muziki filam mkoani Iringa wametoa onyo kwa msanii Elizabeth Michael maarufu Lulu aliyetoka kwa dhamana mahabusu kufuati tuhuma ya kesi yake ya mauwaji ya msanii mwezake Stivin Kanumba ,kuwa anapaswa kutumia muda huu kuwa jirani ni kanisa badala ya kupenda starehe za dunia.
Wakizungumza na mtandao huu wa www.francisgodwin.blogspot.com wasanii hao Johari John na Kevin Sanga walisema kuwa dhamana ya Lulu ni mapenzi ya Mungu hivyo mbali ya kutoka mahabusu kwa dhamana bado anapaswa kuishi kwa utulivu zaidi muda wote ikibidi kuanza kuwa karibu na kanisa.
Hata hivyo John alitaka waumini wa madhehebu mbali mbali kuendelea kumwombea msanii huyo ili Mungu aendelee kusimama upande wake.
Wasanii hao walisema kuwa suala la msanii huyo kuendekeza kujirusha kwa sasa asilipe nafasi katika maisha yake na badala yake kumgeukia Mungu zaidi na kuachana na mambo ambayo hayampendezi mwenyezi Mungu.
0 comments:
Post a Comment