Home » » SHERIA YA MIFUGO KUZAGAA MJINI INAPOVUNJWA MANISPAA YA IRINGA

SHERIA YA MIFUGO KUZAGAA MJINI INAPOVUNJWA MANISPAA YA IRINGA



Kijana aliyekuwa akichunga mifugo hiyo akiwa hana shaka
Magari yakipita  kwa shida  eneo hilo kuhofu ng'ombe hapo kuvuka barabara
Pamoja na Halmashauri ya manispaa ya Iringa mkoani Iringa  kuweka sheria ya kuzuia mifugo kuzagaa katikati ya mji wananchi wameendelea kupuuza sheria hiyo kusudi na kugeuza maeneo ya kandokando ya barabara kuu ya Iringa Mbeya kuwa eneo la Malisho ya Mifugo jambo ambalo ni hatari kwa  usalama wa abiria  wanaotumia barabara  hiyo.

Mtandao  huu wa www.francisgodwin.blogspot.com mchana  huu umeshuhudia  kundi kubwa la ng'ombe wakiwa katika malisho  eneo la Bhesania  Ipogolo wakiwa katika malisho huku  wananchi wakihoji uvunjaji  wa  sheria ya Manispaa ya Iringa .

Baadhi ya  wananchi  wameitaka manispaa ya  Iringa  kusimamia  sheria hiyo ya mifugo kwa kuanzisha msako  wa kukamata mifugo inayozagaa mjini ili  kuepusha ajali .
Na Francis Godwin

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa