wananchi wa Ipogolo mjini Iringa wakitazama mita iliyopasuka kutokana na hitirafu hiyo ya umeme
Mlipuko wa umeme wasababisha taharuki kwa wakazi wa Ipogolo katika manispaa ya Iringa jana usiku na kupelekea wananchi kuyakimbia makazi yao kwa muda.
Wananchi hao waliyakimbia makazi yao baada ya kutokea hitirafu ya umeme eneo la Ipogolo na kusababisha mlipuko mkali wa umeme hivyo kupelekea wananchi kuyakimbia makazi yao kwa muda.
Tukio hilo lilitokea majira ya saa 2 usiku na kupelekea mji mzima wa Iringa kukaaa gizani kwa muda wa nusu saa kabla ya shirika la ugavi wa umeme nchini Tanesco kufika eneo hilo na kujaribu kutatua tatizo hilo .
Wakazi wa eneo hilo waliueleza mtandao huu wa www.francisgodwin.blogspot.com kuwa mlipuko huo ulisababishwa na moja kati ya nyaya kubwa za umeme kukatika na kupelekea Transifoma kulipuka japo hakuna madhara yoyote kwa binadamu wala hakuna nyumba iliyoteketea kwa moto
Chanzo: Blog ya Francis Godwin
0 comments:
Post a Comment