Home » » MKURUGENZI MANISPAA YA IRINGA AWAANGUKIA WASIO HESABIWA

MKURUGENZI MANISPAA YA IRINGA AWAANGUKIA WASIO HESABIWA



Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa Teresia Mahongo akihamasisha sensa katika Radio Furaha FM jana


Mtangazaji wa Radio Furaha Fm akiwa kazini


Mtangazaji wa kipindi cha wanawake Radio Furaha Tukusuga James akimuuliza maswali ya sensa mkurugenzi Mahongo


Mkurugenzi wa manispaa Iringa Bi. Theresia Mahongo amewataka wananchi wa Manispaa ya Iringa kutumia vizuri muda uliosalia ili kuweza kuhesabiwa katika zoezi la Sensa ya watu na makazi .

Aidha amesema endapo mwananchi yeyote atakuwa hajahesabiwa mpaka kufikia siku ya kesho afike ofisini kwake Manispaa ili aweze kuandikishwa katika zoezi hilo.

Amesema zoezi hili ni la siku saba na linatarajiwa kuhitimishwa siku ya jumamosi hivyo bado wananchi wanayonafsi ya kutoa taarifa zao.

Akizungumza katika studio za redio Furaha katika kipindi maarufu cha mwanamke na jamii amewataka wanawake wenye watoto wenye ulemavu kutoona aibu kutoa taarifa juu ya watoto wenye ulemavu kwani kila mtoto anazaliwa kwa maksudi maalum

pia amesisitiza kuwa ni vema taarifa zikatilewa na mkuu wa kaya katika kaya husika ili kuepuka kupatikana kwa takwimu zisizo sahihi

Hivyo amesema iwapo mwananchi wa Manispaa ya Iringa anatatizo ama hajahesabiwa mpaka sasa anaweza kupiga namba 0784476944 ili aweze kuhesabiwa kabla ya muda haujakwisha.

Wakati huo huo mkurugenzi huyo amekemea tabia ya baadhi ya wananchi wa Manispaa ya Iringa kuchoma moto madampo ya kuhifadhia takataka
Chanzo: Blog ya Francis Godwin, Mzee wa matukio Daima

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa