Na Francis Godwin
Watu watatu wamekufa wengine 10 kujeruhiwa katika ajali mbili zilizotokea jana na juzi katika wilaya ya Mufindi mkoani Iringa.
Katika ajali ya kwanza iliyotokea usiku wa kuamkia jana Pamela S.Mbise anayekadiliwa kuwa na miaka kati ya 30 ambaye ni mke wa mfanyakazi wa Sao Hill Mufindi na dereva Taxi mjini Mafinga Edward Mgina pia anakadiliwa kuwa na miaka kati ya 30 na 31 wamekufa papo hapo baada ya gari aina ya RAV 4 ambayo walikuwa wakitumia kusafiriki kuacha njia na kutumbukia katika mto Ruaha eneo la Misitu ya Sao Hill wilayani Mufindi .
Mashuhuda wa tukio hilo waliueleza mtandao huu wa www.francisgodwin.blogspot.com kuwa watu hao walikuwa wakitokea mjini Mafinga kwenda Sao Hill na baada ya kufika eneo hilo gari lao lilitumbukia mtoni na kushindwa kujiokoa baada ya gari hilo kugeuka mataili juu kutokana na kina kirefu cha maji katika eneo hilo na hivyo gari hilo kuonekana baada ya kupita masaa takribani mawili toka walipo zama katika mto huo.
0 comments:
Post a Comment