Mjasiriamali Iringa akionyesha mafanikio yake ya kutengeneza bidhaa mbali mbali kwa kutumia chuma
Wajasirimali wa ushonaji walivyoweza kuboresha kazi zao na kuongeza mitaji yao kutokana na uwezeshaji wa DBG
Suti kali kama hii inashinwa na wajasiriamali wa DBG Iringa
MJasiriamali aliyenufaika na DBG Iringa
Viatu vyenye ubora wa hali ya juu vikiwa vimetengenezwa na mjasiriamali wa DBG Iringa
Wengi wanaongeza kiwango cha ufugaji kuku kupitia DBG Iringa
TPSF -DBG inavyowakomboa wajasiriamali Iringa
Ufugaji bora na wakisasa ulivyoongezeka Iringa
Wajasiriamali mkoani Iringa wamesema kuwa jitihada zinazofanywa na taasisi binafsi ya PTSF- DBG hapa nchini zimeendelea kuwakomboa kiuchumi kwa wao kuongeza kasi ya uzalishaji zaidi .
Wakizungumza mara baada ya sherehe fupi ya kukabidhiwa hundi yenye thamani ya Shilingi milioni 67.4 mjasiriamali Michael Mlole alisema kuwa pamoja na awali kuanza katika hali ya kusuasua kazi hiyo ya ujasiriamali ila baada ya kupatiwa mafunzo ya DBG na kuwezesha wameendelea kukua zaidi kibiashara na hivyo kupongeza taasisi hiyo kwa kazi nzuri inayoendelea kuifanya hapa nchini.
Kwani alisema kuwa hivi sasa wajasiriamali hao ambao awali walikuwa wakiitwa ni wajasirimali wadogo kwa sasa wao wanajiona kuwa ni wafanyabiashara wakubwa kutokana na uwezeshaji unaofanyika chini ya DBG .
Usikose makala maalum ya jinsi ambavyo DBG ilivyoweza kuwawezesha wajasiriamali mkoa wa Iringa na Tanzania bara na Visiwani ,makala itakayokujia hivi karibuni katika mtandao huu
Picha na Habari na Francis Godwin
Picha na Habari na Francis Godwin
0 comments:
Post a Comment