KUTOKA JIMBO LA MAFINGA: MBUNGE WA JIMBO LA MAFINGA AKABIDHI MITUNGI 60 YA GESI KWA WATENDAJI WA KATA

“Lengo la kugawa nishati hii safi ya kupikia ni kuunga mkono juhudi za Kinara wa Nishati Safi ya Kupikia Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ili kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi. Nategemea Watendaji wa Kata Mitaa na Vijiji ndo wenye watu hadi ngazi ya chini kupitia njia hii watakuwa mabalozi wazuri wa matumizi ya nishati safi ya kupigia.”Kauli hiyo imetolewa na Mbunge Wa Jimbo la Mafinga Mjini na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje Mheshimiwa Cosato Chumi alipokuwa akikabidhi mitungi 60 ya gesi kwa Watendaji wa Kata, Mitaa na Vijiji wa Jimbo la Mafinga Mjini lengo likiwa ni kusambaza matumizi Ya Nishati Safi ya kupikia na kuunga mkono juhudi...

KUTOKA MUFINDI: 'UKIKOSA MKOPO AWAMU HII SUBIRI' - DC MUFINDI

“Nawaomba sana Sikilizeni vigezo vilivyowekwa, umekosa awamu hii awamu ijayo hakikisha unapata kwa kufuata vigezo vilivyowekwa,tusiwe wabishi lazima tufuate vigezo.Fedha zinatolewa kila baada ya miezi mitatu kama umekosa awamu hii hakikisha unafuata vigezo na kuandika andiko vizuri ili upate mkopo kwa awamu inayofuata” DC- Mufindi Mheshimiwa Dkt Linda Salekwa.Mhe. Linda amesema Serikali ipo kusimamia kila mwenye vigezo vya kupata mkopo anapata  na kuhakikisha haki inatendeka kwa kila muombaji, wa Mikopo hii ya asilimia 10.Amesema Lengo la Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni Kuhakikisha mikopo inawanufaisha wananchi waliolengwa ili...

KUTOKA MUFINDI: MKUU WA WILAYA YA MUFINDI DKT LINDA SELEKWA AZINDUA ZOEZI LA UGAWAJI WA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI HALMASHAURI YA MJI MAFINGA

Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Mheshimiwa Dkt Linda Selekwa  amezindua zoezi la ugawaji wa mikopo ya asilimia kumi kwa vikundi 62 vya wanawake ,vijana na watu wenye ulemavu katika Halmashauri ya Mji Mafinga ambapo jumla ya shilingi milioni 895,367,600 zimetolewa kwa vikundi hivyo.Mheshimiwa  Dkt Linda Selekwa amewataka wanufaika wa mikopo hiyo kuhakikisha wanatumia fedha hizo katika kukuza na kuendeleza biashara na miradi ambayo wamekuwa wakiifanya na kuachana kujaribu kufanya kitu kipya ambacho kitawapotezea fedha hizo kwa sababu fedha hizi ni za Serikali na zinatokana na mapato ambayo tunalipa kwenye Halmashauri hivyo tunawajibu wa kusimamia...

TUSOME MAGAZETI YA LEO KUTOKA MKOA WA IRINGA

Magazeti   &nb...

JITOKEZENI KUJIANDIKISHA KATIKA DAFTARI KUPIGIA KURA

“ Hakikisheni hizi siku 4 zilizobaki za Uandikishaji Wapiga kura kwaajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wananchi wanajitokeza kwa wingi ili kuandikishwa katika daftari na waweze kutumia haki yao ya msingi tarehe 27 Novemba kuchagua viongozi wanaowataka na mawakala wa vyama vya siasa wanachama wenu hakikisheni wanaandikishwa katika Daftari asibaki hata mwananchi mmoja hajaandikishwa Mwenye sifa ya kuandikishwa”Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Idara ya Serikali za Mitaa OR- TAMISEMI Bi. Angelista Kihaga alipotembelea baadhi ya vituo vya Uandikishaji wapiga kura katika Halmashauri Ya Mji Mafinga lengo likiwa ni kuona hali ya Uandikishaji...

USIMAMIZI WA MIRADI YA MAENDELEO

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Mafinga Bi. Fidelica Myovella ameendelea na kusimamia Miradi ya Maendeleo kwa kuhakikisha inakamilika kwa Ubora wa fedha zinazotumika na kwa wakati.Akiwa ameambatana na baadhi ya Wakuu wa Idara akiwepo Afisa Elimu Sekondari Mwalimu Stephen Shemdoe leo tarehe 14/9/2024  Bi. Myovella amesimamia na kutembelea Ujenzi wa bweni la Wasichana katika Shule ya Sekondari JJ Mungai ambapo ujenzi upo hatua  lenta.Aidha amekagua Ujenzi wa vyumba vitatu  vya madarasa katika Shule ya Msingi Kilimani ambapo maadalizi ya Upauaji yanaendelea.Akiwa katika zoezi hilo la Usimamizi wa Miradi hiyo amewaagiza Idara husika...

TASAF YAMUWEZESHA MNUFAIKA MWENYE UONI HAFIFU KULETA BIDHAA KATIKA MAONESHO YA NANE NANE MBEYA 2024.

Na Sima BingilekiAfisa Habari Mafinga Tc“ Kwa kweli tunaishukuru Serikali  ya Awamu ya Sita ya Mama Samia Suluhu Hassan kipitia TASAF tumeweza kushiriki Maonesho haya ya Nane Nane Jijini Mbeya kwani tumeleta majiko ya kupikia ya udogo tuliyoyafinyanga wenyewe,Hatujawahi kuwaza kuwa kuna siku na sisi tutafika Mbeya kwenye Maonesho haya na kuleta bidhaa zetu , Tunaishukuru sana Serikali”Kauli hiyo imetolewa na Wanufaika wa TASAF kutoka katika Halmashauri ya Mji Mafinga wilaya ya Mufindi Bi Roida Mgwale(40) Mkazi wa Rungemba na Bi Honorina Nyongole(40) Mkazi wa Rungemba Mafinga mwenye Uoni Hafifu na mfinyanzi wa vyungu na majiko ya Udongo.“Mimi...

MRADI WA SLR WATENGA EKARI 28,000 UREJESHAJI UOTO WA ASILI

Ofisi ya Makamu wa Rais kupitia Mradi wa Urejeshwaji Endelevu wa Mazingira na Hifadhi ya Bayoanuai Tanzania (SLR) imetenga ekari 28,000 za misitu ya jamii iliyopo katika vijiji vya Halmashauri saba (07) kwa ajili ya urejeshaji wa uoto wa asili.Hayo yamebainishwa Julai 31, 2024 Mkoani Iringa na Mratibu wa Kitaifa wa Mradi wa SLR, Dkt. Damas Mapunda wakati wa mahojiano na waandishi wa vyombo vya habari katika kikao cha siku moja cha kamati ya kitaifa ya usimamizi wa mradi kilichopokea taarifa ya mradi huo.Dkt. Mapunda amesema tangu kuanza kwa mradi mwaka 2021, wataalamu walibainisha baadhi ya maeneo yaliyopo ndani ya halmashauri zinazotekeleza...

USAJILI WA WAKULIMA KIDIJITALI WAFIKIA ASILIMIA 64.7

Na Alex Nelson MalangaAfisa Habari----Mji MbingaMbinga.  Usajili wa wakulima kidijitali katika Halmashauri ya Mji wa Mbinga umefikia asilimia 64.7, taarifa kutoka Idara ya Kilimo ya  Halmashauri hiyo inaonesha.Taarifa kutoka idara hiyo inaonesha kuwa tangu zoezi la usajili lianze katika msimu wa kilimo wa 2022/23, tayari wakulima 23,222 kati ya 35,876 wamejisajili katika mfumo huo wa kidijitali.Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Mbinga Dkt. Kung’e Nyamuryekung’e Ijumaa ya Julai 26 alisema kuwa kwa kujisajili kidijitali, wakulima wataweza kupata huduma mbalimbali kiurahisi.Alisema miongoni mwa huduma ambazo wakulima watapata kupitia...

ELIMU YA KUZUIA MOTO YATOLEWA KWA WAJUMBE SERIKALI YA KIJIJI CHA RUNGEMBA- IRINGA

Elimu ya kuzuia Moto imetolewa kwa Serikali ya Kijiji Cha Rungemba lengo likiwa ni kutoa tahadhari ya moto hasa katika kipindi hiki cha Kiangazi ambacho kina upepo mkali na wananchi wanasafisha mashamba kwaajili ya kilimo.Akizungumza Mkuu wa Kitengo Cha Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira Ndugu. Demitrius Kamtoni akiwa ameambatana na Wataalumu kutoka kitengo hicho amesemaNi muhimu vibali kutolewa na Serikali za vijiji husika kwa  mwananchi anayetaka kusafisha shamba kwa njia ya moto ili tahadhari zote za Moto zichukuliweAidha Ndugu Kamtoni amesema Elimu nyingine iliyotolewa kwa wajumbe hao wa Serikali ya Kijiji cha Rungemba ni:--Sheria ya...

MKURUGENZI SHULE ZA REALHOPE AKABIDHI KOMPYUTA TATU KWA HALMASHAURI YA MJI MAFINGA

“Lengo langu ni kuunga Mkono juhudi zinazofanywa na Serikali hii na naahidi kuendelea kujitolea ili jamii iendelee kunufaika hasa katika Sekta ya Afya na Elimu,  kompyuta hizi 3 (Dell )zitarahisisha uwekaji wa takwimu na utunzaji wa kumbukumbu kidigitali hivyo kupunguza wagonjwa kukaa muda mrefu kusubiri huduma.”Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Shule za Really Hope zilizopo Mji Mafinga Ndugu Dickson Mwipopo alipokuwa akikabidhi kompyuta 3 aina ya Dell zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 5 kwa Mkurugenzi Mji Mafinga Bi , Fidelica Myovella kwaajili ya matumizi ya Sekta ya Afya.Akipokea compyuta hizo Mkurugenzi Mji Mafinga akiwa...

SALAMU ZA PONGEZI

Baraza la Waheshimiwa Madiwani, Timu ya Menejimenti na watumishi wote wa Halmashauri ya Mji Mafinga wanakupongeza  Mbunge wa Jimbo la Mafinga Mjini Mheshmiwa Cossato Chumi  kwa kuteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki HONGERA SANA MAFINGA IPO SAL...

NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA MJI MAFINGA- 2024

...
 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa