Home » » HALMASHAURI YA MJI MAFINGA YAPITISHA RASIMU YA BAJETI YA MAENDELEO KIASI CHA SHILINGI BILIONI 25.9 KWA MWAKA WA FEDHA 2018-2019

HALMASHAURI YA MJI MAFINGA YAPITISHA RASIMU YA BAJETI YA MAENDELEO KIASI CHA SHILINGI BILIONI 25.9 KWA MWAKA WA FEDHA 2018-2019

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 





Halmashauri ya mji wa Mafinga imepitisha rasimu hiyo ya bajeti ya maendeleo katika  kikao cha baraza la waheshimiwa madiwani kilichofanyika 26/2/2018 katika ukumbi wa halmashauli ambapo jumla ya fedha kiasi cha shilingi bilioni 25.9 zilipitishwa. 
Akiwasilisha rasimu hiyo ya bajeti kwa wajumbe wa kikao hicho kwa niaba ya mkurugenzi  Afisa mipango wa halmashauri ndugu Andambike kyomo amesema halmashauri ya mji wa mafinga imejipanga katika kuboresha namna ya utoaji wa huduma bora kwa wananchi kwa kujikita katika vipaumbele vitano vya halmashauri ambavyo ni kuboresha makusanyo mapato ya ndani ili kujenga stendi ya kisasa eneo la kinyanambo na kuboresha mazingira ya uwekezaji na ujenzi wa viwanda,pili ni kuboreshakwa kutenga fedha ili kugharamia uendeshaji ujenzi na ukarabati wa vituo vya kutolea huduma za afya na elimu.

Afisa mipango ndugu Kyomo  alindelea kuwasilisha kipaumbele cha tatu kuwa ni kuboresha utendaji kazi wa watumishi wa umma kwa kutenga fedha kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya kufanyia kazi,ujenzi wa nyumba za watumishi na kutenga fedha za mishahara kwa kuzingatia ikama wakati kipaumbele cha nne ni kuboresha uratibu, usimamizi na utekelezaji wa shughuli mbalimbali  zinazotolewa na halmashauri kwa wananchi kwa kutenga fedha za kutosha kwa ajili ya ununuzi wa magari matatu (3) ya kuimarisha usimamizi na ufuatiaji huku kipaumbele cha tano ikiwa ni kuimarisha utawala bora kwa kufanya vikao vya kisheria vya halmashauri na kuimarisha mifumo ya  utendaji.

Lengo kuu la bajeti ni kutekeleza malengo ya dira ya Taifa ya maendeleleo 2025 na malengo ya milenia na mpango wa maendeleo endelevu (SDG’s) ambapo kwa pamoja yanaelekeza kupunguza umasikini iliokithiri na njaa,elimu ya msingi kwa wote,usawa wa kijinsia,kupunguza vifo vya watoto, kupunguza vifovya uzazi, utunzaji wa mazingira,kukabiliana na janga la UKIMWI na kujenga uchumi imara wenye kuhimili ushindani.

Mambo mengine muhimu yaliyozingatiwa katika uandaaji wa bajeti  ni pamoja na Hotuba ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dk. John Pombe Joseph Magufuli wakati akifungua rasmi Bunge jipya la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania,Dodoma tarehe 20 Novemba 2015 ambayo pamoja na mambo mengine inaelekeza kupunguza kero na kusogeza huduma kwa wananchi.
 

0 comments:

 
Powered by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa