Katibu
Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Ndg. Abdulrahman Kinana amemtumia salamu za
rambi rambi Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa Ndg. Jesca Msambatavangu
kufuatia kifo cha Mhe Joseph Mungai, Mbunge mstaafu wa Jimbo la Mufindi
kilichotokea jana tarehe 08 Novemba, 2016 katika Hospitali ya Taifa ya
Muhimbili jijini Dar es salaam.
Mhe.
Mungai, ameshika nyadhifa mbalimbali za uongozi na utumishi katika
Chama na Serikali. Alikuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC),
Mkuu wa Mkoa, Mbunge kuanzia miaka ya 1970 hadi 2010, na amekuwa Waziri
katika wizara mbalimbali za Serikali ya Jamhuri ya Muungano kuanzia
Awamu ya kwanza mpaka ya nne.
Mhe.
Mungai, atakumbukwa na wanaCCM, na wananchi wa Mkoa wa Iringa na
Tanzania kwa kuasisi na kuendeleza shamba kubwa la miti la SAOHILL na
kwamba mchango wake huo tutaendelea kuuenzi na kuuthamini.
Bwana ametoa na Bwana ametwaa, jina lake lihimidiwe.
Imetolewa na:-
Christopher Ole Sendeka (MNEC)
MSEMAJI WA CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM)
09.11.2016
0 comments:
Post a Comment