Na MatukiodaimaBlog
MKUU wa mkoa
wa Iringa Amina
Masenza ameipongeza kazi kubwa
inayofanywa na kamati ya usalama barabara
mkoa wa Iringa chini ya
mwenyekiti wa kamati hiyo Salim
Abri Asas ambae amekuwa ni msaada mkubwa katika kuokoa maisha ya watanzania
wanaopata ajali ndani ya mkoa kwa
kujitolea misaada mbali mbali ikiwemo ya dawa na usafiri.
Akitoa pongezi hizo
leo wakati wa maadhimisho ya wiki
ya nenda kwa usalama ambayo imeadhimishwa
kimkoa katika viwanja vya stendi
ya mabasi yaendayo mikoani mjini
Iringa ,mkuu huyo wa mkoa alisema mbali ya
kuwepo kwa wadau mbali mbali
katika kupunguza ajali na kusaidia pindi ajali
zinapotokea ila serikali
yake ngazi ya mkoa inatambua mchango mkubwa unaotolewa na familia ya mfanyabiashara Asas
katika kusaidia kuokoa roho za watanzania
pindi wanapopatwa ajali.
“ Kana mambo mengi
makubwa ambayo Asas amekuwa
akijitolea kuyafanya kwa ajili
ya kunusuru maisha ya majeruhi wanaopatwa na ajali ndani ya
mkoa wetu mfano katika ajali iliyotokea Changalawe Mafinga kwa kuhusisha basi la Majinja ajali
iliyoua watu zaidi
ya 50 na kujeruhi wengine wengi …msaada mkubwa wa
kuokoa roho za majeruhi kwa kujitolea dawa zilionyeshwa na Asas ….mimi
nikiwa ni mkuu wa mkoa na serikali
ya mkoa tunapongeza kazi nzuri ya
Asas na familia yake katika
kuwaidia kuokoa roho za majeruhi naomba Mwenyezi Mungu azidi kumuongezea pale anapopunguza kwa ajili ya wengine”
Alisema kuwa wiki ya
nenda kwa usalama ni kwa ajili ya kukumbushana
mema yanayohusu kufuata sheria
na kanuni za usalama barabarani ili kuondoa vifo
vinavyotokana na ajali barabarani
hivyo pamoja na kumbushana
kanuni na sheria za usalama barabarani
ni vema
kutumia maadhimisho hayo kutambua
michango mbali mbali ya
wadau wanaojitolea kwa jili ya
kufanikisha elimu ya usalama bararani
ama kusaidia kuokoa majeruhi na vinginevyo.
“ Kumekuwepo na ongezeko
kubwa la ajali za barabarani zinazohusisha pikipiki
ajali hizi zinaweza kuepukika endapo waendesha
na wapanda pikipiki watazingatia
sheria na kanuni za usalama barabarani ….natoa wito
kwa wapanda pikipiki kuacha tabia ya
kuendesha bila kupata mafunzo na kutokuwa na leseni suala la
kuvaa kofia ngumu kwa madereva na
abiria ni lazima …..acheni tabia ya kubeba abiria zaidi ya mmoja (mshikaki) …..pia kuacha kunywa
pombe vikiwemo viroba wakati wa kutoa
huduma ya usafiri …..kweli naumia
sana kuona vijana wanakufa baada ya kuendesha
pikipiki huku wakiwa
wamelewa viroba”alisema mkuu huyo wa
mkoa
Kwa watumiaji wengine
wa barabara ni vema kuzingatia sheria
za usalama barabarani kwa
kufunga mikanda pindi
wanapokuwa katika magari pia
abiria kuacha kushabikia mwendo kasi na badala yake kuwafichua madereva wanaokiuka
sheria za usalama barabarani.
Hata hivyo mkuu
huyo wa mkoa aliagiza
jeshi la polisi kikosi cha
usalama barabarani kuwakamata
waendesha boda boda wote
wanaoendesha boda boda kwa vurugu
na baadhi yao kushitua watu kwa
kuifanya boda boda hiyo kutoa mlio mkali mfano wa bomu .
Aidha alitaka
kuanzia sasa dereva
boda boda atakayebainika kusababisha ajali na kuita
wenzake kwa ajili ya kumfanyia vurugu aliyesababishiwa ajali kukamatwa na
washiriki wake na kufikishwa
mahakamani .
Kwa upande wake mwenyekiti wa
kamati ya usalama barabarani
mkoa wa Iringa Salim Abri alisema
kuwa kuna dhana
potofu kwa baadhi ya watu
kufikiri suala la usalama barabarani
linahusu ajali pekee yake kwani
hata kupiga honi bila
sababu ama kukwamisha shughuli za
barabara kwa mambo binafsi
pia ni kero kwa watumiaji
wengine wa barabara .
“Tunapozungumzia
sheria za usalama barabani sit u kwa ajili ya kuepusha ajali ila ni pamoja na kuepusha kero
za usalama barabarani baadhi yetu
tumekuwa tukifikiri usalama
barabarani ni kuepusha ajali tu ila
ukweli ukizingatia usalama barabarani ni
pamoja na kero kubwa ya kutozingatia
sheria za usalama barabarani hata kupiga
honi bila sababu ni kero…..”
Alisema katika watumiaji wa
vyombo vya moto
wanaoongoza kwa kuvunja
sheria za usalama barabrani na kero nyingine za
barabarani ni boda boda hivyo angependa kuwaomba
waendesha boda boda kupunguza
kero za usalama barabarani
zikiwemo za kupiga honi ovyo na ajali zinazoweza kuepukika .
Katibu wa kamati ya
usalama barabarani mkoa
wa Iringa ambae ni mkuu wa kikosi cha usalama barabarani mkoa (RTO) Leopold Fungu alisema kuwa
kwa mujibu wa tathimini ya jail za barabarani kwa kipindi
cha miezi tisa mwaka 2015
ikilinganishwa na kipindi kama hicho cha
mwaka huu 2016 mkoa wa Iringa
umefanikiwa kwa kiasi
kikubwa kupunguza ajali za
barabarani .
Kuwa kwa kipindi cha January
hadi Septemba mwaka 2015 ajali
zilikuwa ni 41 ila kwa kipindi
cha January 2016 hadi septemba 30
ni ajali 35 ndizo
zilizotokea wakati watu
waliopoteza maisha kwa kipindi cha January 2015 hadi Septemba ilikuwa ni 34 ila kwa
mwaka huu toka January hadi Septemba 30 ni
watu 30 ndio waliopoteza maisha aidha katika
kipindi hicho ajali za
piki piki zimepungua kwa asilimia
15 huku watu waliokufa kwa ajili ya pikipiki wamepungua kwa asilimia 11 na
waliojeruhiwa wamepungua kwa asilimia 20 kuwa
kupungua kwa matukio ya ajali ni
kutokana na elimu za mara kwa mara.
|
0 comments:
Post a Comment