Baadhi ya walimu wakijitambulisha kwa waalikwa |
Baadhi ya wazazi wakipata maelezo kwa wanafunzi hao |
Wazazi wakitazama jinsi wanafunzi hao walivyobobea katika kompyuta |
Wanafunzi wa Chekechea 31 waliohitimu wakionyesha maonyesho ya masomo |
Wanafunzi wa shule hiyo wakionyesha maonyesho ya masomo wakati wa mahafali ya chekechea |
Baadhi ya wazazi waaosomesha watoto wao shule ya Southern Highlands Mafinga |
Mkuu wa shule ya Southrn Highlands Mafinga Joson Nyangwara akisoma taarifa ya shule hiyo mbele ya wazazi |
Wanafunzi wa chekechea wakisoma risala yao |
Mjumbe wa bodi ya shule ya English Medium ya Southern Highlands Mafinga mkoani Iringa Marcelina Mkini akimpongeza mmoja kati ya wanafunzi wa shule hiyo kwa kufanya vizuri katika masomo yake jana wakati wa mahafali ya Chekechea na kikao cha wazazi shuleni hapo |
Diwani wa Luhunga kushoto akiwa na diwani wa kasanga baada ya kukutana shule ya Southern Highlands Mafinga kushiriki kikao cha wazazi |
Magari ya baadhi ya wazazi wanaosomesha watoto wao shule ya Southren Highlands Mafinga yakiwa yameegeshwa nje ya shule hiyo |
Mgeni rasmi Daniel Mwaisela akikabidhiwa zawadi toka kwa uongozi wa shule ya Southern Hihglands Mafinga
Na MatukiodaimaBlog
SERIKALI wilayani Mufindi mkoani
Iringa imepongeza kasi ya ufundishaji ya walimu wa shule binafsi ya
Southern Highlands Mafinga na kuwataka walimu
wa shule zote kuiga mfano wa walimu wa shule ya southern Highlands Mafinga ili kuiwezesha wilaya hiyo
kuwa na shule bora nyingi zaidi .
Kuwa jitihada zinazoonyeshwa na walimu wa shule ya
Southern Highklands Mafinga ambazo zimekuwa
zikiifanya shule hiyo kuendelea
kuongoza mitihani ya Kitaifa ya darasa la saba kila mwaka zinapaswa kuonyeshwa
na walimu wa shule nyingine wilayani hapo ili kuipa heshima wilaya na mkoa wa Iringa .
Akitoa
pongezi hizo jana kwa niaba ya mkuu wa wilaya mgeni rasmi katika
sherehe za mahafali ya chekechea na
kikao cha wazazi katika shule hiyo ya
Southern Highlands Mafinga katibu tarafa wa Ifwagi Arois
Mtengella alisema wilaya inajivunia sana
na matokeo mazuri ya shule hiyo.
“Shule hii ambayo ni English
Medium imekuwa ikifanya vizuri sana katika
mitihani yake na kitendo cha
wazazi kutoka nje ya wilaya na mkoa
wa Iringa kuleta watoto
wao hapa Mafinga ni moja ya mambo
ya kujivunia …..pia uchumi wa wilaya
yetu unaongezeka kwa wageni hao kuja hapa kwetu maana siku kama hii kila mwananchi mwenye biashara
ameingiza kipato chake”
Pia alisema changamoto kubwa kwa wilaya
ya Mufindi na mkoa wa Iringa
pamoja na kuongoza kwa uzalishaji
wa mazao ya chakula kama mahindi
ila bado watoto
wengi wanatatizo la utapiamlo hivyo kuwataka
wananchi kuongeza jitihada za
kuwapikia watoto wao ugali
wa dona badala ya kukomboa mahindi .
Alisema kitendo
cha watoto kulishwa ugali wa mahindi
yaliyokobolewa na kulowekwa ni
kuwafanya kuwa na afya duni
na hivyo
uwezo wao darasani huwa mdogo
zaidi .
Mkuu huyo
wa wilaya alisema kuwa
elimu bora ni pamoja na
lishe nzuri kwa watoto na
kuwa wazazi lazima
wahakikishe watoto wao
wanawapa lishe bora ili
kuwaongezea uwezo wa
kufundishika .
Kwa
upande wake mwalimu mkuu wa Southern
Highlands Mafinga Joson Nyangwara akizungumza kwa niaba ya mkurugenzi
mtendaji wa shule hiyo Mary Mungai alisema kuwa shule imekuwa na utaratibu wa kukutana
na wazazi na walezi wa wanafunzi wanaosoma shuleni hapo
mara baada ya matokeo ya kitaifa ya mtihani wa darasa
la saba ili kupokea maoni yao mbali mbali kwa
ajili ya maendeleo ya shule hiyo .
Mkuu
huyo alisema moja kati ya mafanikio ya shule hiyo
kuendelea kufanya vizuri katika mitihani ya taifa
ya darasa la saba kila mwaka ni kutokana na ushirikiano
mzuri uliokuwepo kati ya wazazi na walimu na kuwa
kupitia vikao vya pamoja kati ya wazazi na uongozi wa
shule mapungufu yanayojitokeza yamekuwa yakifanyiwa kazi
pasipo watoto kupata vikwazo katika masomo yao.
Hivyo
alisema kwa mwaka huu wanafunzi wote 51 waliofanya mtihani wa
Taifa wa darasa la saba wamefaulu kujiunga na kidato cha kwanza mapema
mwakani jambo ambalo linaendelea kuwavuta wazazi wengi
zaidi kupeleka watoto wao shuleni
hapo .
Kuwa mwaka huu 2016 jumla ya wanafunzi 51 walisajiliwa kufanya mtihani wa darasa la saba na wote walifanya wastani wa shule 185.3137 kundi la shule watahiniwa 40 au zaidi ambapo imeweza kuongoza kiwilaya kuwa ya kwanza na kimkoa ya 6 kati ya shule 232 katika mkoa wa Iringa na shule ya 198 kati ya shule 8109 kitaifa .
Alisema
kuwa toka shule hiyo ilipoanzishwa mwaka 1994 kama Day
Care na Pre-school na mwaka 1997 kuanza shule ya msingi imekuwa ikifanya
vizuri na hakuna mtoto aliyepata kufeli .
“Shule
yetu mwaka 2001 shule ilitoa wanafunzi wa kwanza wa darasa la Saba na wanafunzi
walikuwa 17, wote walifaulu vizuri na wote walichaguliwa kuendelea na masomo ya
kidato cha kwanza”
Shule
hiyo inapenda kuwatangazia wazazi kote nchini ambao wanatafuta shule bora
kwa ajili ya watoto wao kuwa nafasi bado zipo na kuwa wanapokea
watoto wa chekechea ,darasa kwanza ,pili ,tatu na tano wanaotoka
shule za kawaida kiswahili au English medium
kwa darasa la nne na sita lazima wawe wanatoka shule za english medium tu
usahili
unafanyika tarehe 10/12/2016 shuleni Mafinga na baada ya hapo
itakuwa kila siku ya kazi kuanzia saa 2 asubuhi hadi saa 9 alasiri
Mjumbe wa
bodi ya shule
hiyo Marcelina Mkini alisema kuwa
kwa ajili ya uwekezaji wa kweli ni
vizuri wazazi kuwekeza
pesa zao kwa kusomesha
watoto badala ya kuweka pesa benk
Alisema kuweka
pesa benk pasipo kusomesha
watoto ni bure kwani mwisho wa
siku fedha hizo huleta ugomvi wakati mzazi unapokufa ndugu huanza
kugombaniana na kuwaacha watoto masikini.
|
.
|
0 comments:
Post a Comment