Home » » CHUO KIKUU IRINGA WAMPONGEZA RAIS DKT MAGUFULI KWA UHAKIKI WA WATUMISHI HEWA

CHUO KIKUU IRINGA WAMPONGEZA RAIS DKT MAGUFULI KWA UHAKIKI WA WATUMISHI HEWA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
                                                           Rais Dkt John Magufuli 

 Wahitimu   Aziza Mkawa na Amina Ally  wakimlisha  keki  mwenzao Eugenia Msahala aliyehitimu jana  chuo  kikuu  cha Iringa

Wahitimu  wa chuo  kikuu cha Iringa  Rubeny Nyagawa kulia ,Anna Laiza , Deodatus Mnyang'ari na Anna Lwanda wakijipongeza kwa  keki baada ya  kuhitimu digirii  ya  biashara  na utawala katika  chuo  kikuu cha Iringa
 Na MatukiodaimaBlog
UONGOZI  wa  Chuo kikuu cha Iringa (UoI) umepongeza   jitihada  zinazofanywa na  serikali ya  awamu ya  tano  chini  ya Rais  Dkt John  Magufuli juu ya uhakiki wa   watumishi  hewa wenye  vyeti  feki kwa madai  hatua   hiyo  ni  nzuri  itasaidia kupata  wataalam wenye  sifa sahihi   tofauti na  ilivyokuwa  awali kuwa na utitiri  wa   watumishi  wasio na uwezo.


Pongezi  hizo  zimetolewa jana   wakati wa  mahafali ya chuo  hicho na mwenyekiti wa Bodi ya Chuo,  askafu  wa kanisa la  kiinjili  la kilutheri Tanzania (KKKT) dayosisi ya  Iringa  Dkt. Odenburg  Mdegela alisema kuwa zoezi hilo linapembua mchele na chuya na kuwaacha wale wenye vyeti halai tu.

Alisema ilikuwa si sahihi mmoja akae darasani miaka mitatu na mwingine apate cheti kutoka kariakoo tena kikiwa a ufaulu wa juu kuliko Yule aliyekaa darasani.


Dkt. Mdegela alisema watu hawa wanapokutana kazini Yule alipata vyeti bandia vyenye ufaulu wa hali ya juu anakuwa hajui kazi jambo lililokuwa likirudisha nyuma maendeleo ya taasisi nyingi na nchi kwa ujumla.


“Uhakiki wa vyeti unapaswa kuungwa mkono na wadau wote wakiwemo wa elimu kwa kuwa hali ilikuwa mbaya huku wale wenye vyeti badia vikiwa na ufaulu wa hali ya juu ilhali hawajui kazi”, alisema Dkt. Mdegela


Aidha alisema Chuo hicho kinajipanga kuachana na mtazamo uliojengeka kwa muda mrefu wa kujiendesha kwa kutegemea wafadhili mbalimbali wa ndani na nje ya nchi pamoja na mikopo ya ada za wanafunzi kutoka serikalini.


Alisema wanatarajia kuanzisha Asasi itakayokuwa imeungwanishwa na Chuo ambayp itakuwa ikitoa mikopo kwa ajili ya wanafunzi ambao wamekwama kupata huduma hiyo kutoka maeneo mengine.



Kwa  upande  wake mkuu wa Chuo hicho, Jaji mkuu mstaafu Augustine Ramadhani alisema ni vema wahitimu wakawa wazalendo kwa nchi yao na kuitumia elimu waliyoipata kwa maendeleo ya watanzania wote.


Huku makamu Mkuu wa Chuo hicho Prof Joseph Madumula alisema mazingira ya utoaji wa elimu kwa sasa yamekuwa na ushindani mkubwa tofauti na miaka ya nyuma ambapo kulikuwa na Chuo kikuu kimoja cha Dar es Salaam kikiwa na matawi mawili ya Sokoine na Muhimbili.


Aliongeza kuwa kwa sasa kuna zaidi ya vyuo vikuu 60 vya binafsi na serikali lakini idadi ya wanafunzi wanaodahiliwa haijaongezeka kulingana na vyuo idadi ya vyuo.

Alisema wamejipanga kutoa elimu shirikishi ya ujasiliamali kwa wanafunzi wote wa Chuo hicho ili wakimaliza wasitegemee kuajiriwa tu bali wawe na uwezo wa kujiajiri na kuzalisha ajira kwa vijana wengine.

0 comments:

 
Powered by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa