Rais Dkt John Magufuli
Wahitimu Aziza Mkawa na Amina Ally wakimlisha keki mwenzao Eugenia Msahala aliyehitimu jana chuo kikuu cha Iringa
Wahitimu wa chuo kikuu cha Iringa Rubeny Nyagawa kulia ,Anna Laiza ,
Deodatus Mnyang'ari na Anna Lwanda wakijipongeza kwa keki baada ya
kuhitimu digirii ya biashara na utawala katika chuo kikuu cha
Iringa
Na MatukiodaimaBlog
UONGOZI wa
Chuo kikuu cha Iringa (UoI) umepongeza jitihada zinazofanywa na
serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dkt John Magufuli juu ya
uhakiki wa watumishi hewa wenye vyeti feki kwa madai hatua hiyo
ni nzuri itasaidia kupata wataalam wenye sifa sahihi tofauti na
ilivyokuwa awali kuwa na utitiri wa watumishi wasio na uwezo.
Pongezi hizo zimetolewa jana wakati wa mahafali ya chuo hicho na mwenyekiti wa Bodi
ya Chuo, askafu wa kanisa la kiinjili la kilutheri Tanzania (KKKT) dayosisi ya Iringa Dkt. Odenburg Mdegela
alisema kuwa zoezi hilo linapembua mchele na chuya na kuwaacha wale wenye vyeti
halai tu.
Alisema ilikuwa si sahihi mmoja akae darasani miaka mitatu
na mwingine apate cheti kutoka kariakoo tena kikiwa a ufaulu wa juu kuliko Yule
aliyekaa darasani.
Dkt. Mdegela alisema watu hawa wanapokutana kazini Yule
alipata vyeti bandia vyenye ufaulu wa hali ya juu anakuwa hajui kazi jambo
lililokuwa likirudisha nyuma maendeleo ya taasisi nyingi na nchi kwa ujumla.
“Uhakiki wa vyeti unapaswa kuungwa mkono na wadau wote
wakiwemo wa elimu kwa kuwa hali ilikuwa mbaya huku wale wenye vyeti badia
vikiwa na ufaulu wa hali ya juu ilhali hawajui kazi”, alisema Dkt. Mdegela
Aidha alisema Chuo hicho kinajipanga kuachana na mtazamo
uliojengeka kwa muda mrefu wa kujiendesha kwa kutegemea wafadhili mbalimbali wa
ndani na nje ya nchi pamoja na mikopo ya ada za wanafunzi kutoka serikalini.
Alisema wanatarajia kuanzisha Asasi itakayokuwa
imeungwanishwa na Chuo ambayp itakuwa ikitoa mikopo kwa ajili ya wanafunzi
ambao wamekwama kupata huduma hiyo kutoka maeneo mengine.
Kwa upande wake mkuu wa Chuo hicho, Jaji mkuu mstaafu Augustine
Ramadhani alisema ni vema wahitimu wakawa wazalendo kwa nchi yao na kuitumia
elimu waliyoipata kwa maendeleo ya watanzania wote.
Huku makamu Mkuu wa Chuo hicho Prof Joseph Madumula alisema
mazingira ya utoaji wa elimu kwa sasa yamekuwa na ushindani mkubwa tofauti na
miaka ya nyuma ambapo kulikuwa na Chuo kikuu kimoja cha Dar es Salaam kikiwa na
matawi mawili ya Sokoine na Muhimbili.
Aliongeza kuwa kwa sasa kuna zaidi ya vyuo vikuu 60 vya
binafsi na serikali lakini idadi ya wanafunzi wanaodahiliwa haijaongezeka
kulingana na vyuo idadi ya vyuo.
0 comments:
Post a Comment