Home » » RAIS WA WACHIMBA MADINI AJITOSA KUMSAIDIA RAIS DR MAGUFULI

RAIS WA WACHIMBA MADINI AJITOSA KUMSAIDIA RAIS DR MAGUFULI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

 Rais  wa  shirikisho la  wachimbaji madini Tanzania (FEMATA ) Bw  John Bina  akitambulishwa  mbele ya  balozi wa China nchini (hayupo pichani) kulia ni waziri wa Kilimo ,Mifugo na uvuvi Bw Mwigulu Nchemba
 Bw  John Bina  akihamasisha uchangiaji wa madawati  mashuleni

  balozi  wa Chini Nchini Tanzania Dr Lu  Yonq.ng  katikati  akiwa na viongozi wa mkoa wa Shingida  kutoka  kulia mkuu wa  mkoa wa Singida Bw Methew Mtigumwe,waziri wa  kilimo ,Mifugo na Uvuvi Bw Mwigulu Nchemba ,mbunge wa  viti maalum mkoa wa Singida Bi Martha Mlata  na Rais wa FEMATA Bw John Bina

Na MatukiodaimaBlog ,

RAIS wa shirikisho la vyama vya   wachimbaji    madini Tanzania (FEMATA) ametoa wito kwa wachimbaji wote  yakiwemo makampuni makubwa ya uchimbaji   wa madini  kujitokeza kumuunga mkono  Rais Dr John Magufuli   katika harambee ya kuchangia madawati kwa shule mbali mbali hapa nchini.

Huku akisifu  mwitikio mzuri  wa kampuni ya Sunshine Minning  kwa  kuunga kuitikia wito  huo kwa  kuchangia madawati 100 yenye thamani ya Tsh milioni 85,000 kwa Halmashauri ya wilaya ya Iramba mkoani Singida  .

Akizungumza na  waandishi wa  habari jana ,Rais  wa FEMATA  John Bina alisema  kuwa Shirikisho  lake  limelazimika  kumsaidia Rais Dr Magufuli kuhamasisha uchangiaji wa madawati  kwa  wanachama  wake ili kumaliza kabisa tatizo  hilo la uhaba  wa madawati  na  kuona   sekta ya  elimu nchini  inaboresheka  zaidi  kwa   kuhakikisha  wanafunzi  hawakai chini.

Bw Bina  alisema  kuwa katika   kuunga mkono  jitihada za  serikali wao kama sehemu ya  wadau wa maendeleo katika Taifa hawakupenda  kuwa  nyuma kujitokeza  kuchangia madawati hasa  ukizingatia  kuwa elimu  bora  ni mwanzo wa  kuwa na taifa  bora .

"Suala   hili la elimu si la  serikali pekee kila mmoja kwa nafasi yake ana umuhimu katika  kuboresha  elimu  nchini  na si  vema  kwa  kila  jambo  kuitazama  serikali ......serikali  ina  nafasi yake  ila  na sisi  wadau  tuna nafasi  yetu katika  kuiunga mkono serikali pia  wanafunzi  wananafasi yao .... walimu na  wazazi  pia " alisema rais Bina

Hata   hivyo  aliwataka   wadau  wengine  na  wananchi  mmoja  mmoja kwa nafasi yake  kujitokeza kuunga mkono uchangiaji wa madawati  ili  kumaliza kabisa kero  hiyo ya  uhaba wa madawati  mashuleni.

Alisema  wao kama wadau  wa maendeleo  kupitia FEMATA wataendelea  kuunga mkono  jitihada  mbali mbali  zinazoendelea  kufanywa na serikali ya Rais Dr Magufuli  jitihada  zenye  lengo la  kulifanya Taifa   kuzidi  kuwa mbele  kimaendeleo.

Pia  alisema  kwa wadau  wa  sekta   hiyo ya madini  pekee  kama  kila mmoja atajitolea  kuchangia madawati  upo  uwezekano mkubwa wa  zoezi   hilo kukamilika mapema   zaidi na kuwataka  wadau  wengine   mbali ya wale wa madini  nao kwa nafasi  zao  kujitolea madawati  badala ya  kuiachia  serikali pekee.

“ Ninakusudia  kama  Rais  wa FEMATA  kuwakutanisha  wachimbaji  wote mbali na mambo mengine  tutaangalia  ushiriki  wetu katika masuala  ya kijamii yakiwemo ya uchangiaji wa madawati”

Hata   hivyo mkuu  wa  mkoa  wa  Singida Bw Methew Mtigumwe mbali ya  kupongeza harakati  za Rais  huyo wa FEMATA  kwa  kuunga mkono agizo la rais kwa  kujitolea  kuhamasisha uchangiaji wa madawati  bado  alisema  kuwa jambo  hilo ni  jema na linapaswa  kupongezwa zaidi.

Alisema katika mkoa  wa Singida  kila mkuu wa  wilaya ameagizwa  kusimamia utekelezaji wa agizo la Rais la upungufu wa madawati katika eneo lake na  kuwa mkoa umejipanga  kumaliza kabisa  kero  hiyo ya uhaba wa madawati .
MWISHO
KAWAIDA RAIS WA WACHIMBA MADINI AJITOSA RASMI KUMSAIDIA RAIS DR MAGUFULI ........ Rais wa shirikisho la wachimbaji madini Tanzania (FEMATA ) Bw John Bina akitambulishwa mbele ya balozi wa China nchini (hayupo pichani) kulia ni waziri wa Kilimo ,Mifugo na uvuvi Bw Mwigulu Nchemba Bw John Bina akihamasisha uchangiaji wa madawati mashuleni balozi wa Chini Nchini Tanzania Dr Lu Yonq.ng katikati akiwa na viongozi wa mkoa wa Shingida kutoka kulia mkuu wa mkoa wa Singida Bw Methew Mtigumwe,waziri wa kilimo ,Mifugo na Uvuvi Bw Mwigulu Nchemba ,mbunge wa viti maalum mkoa wa Singida Bi Martha Mlata na Rais wa FEMATA Bw John Bina Na MatukiodaimaBlog , RAIS wa shirikisho la vyama vya wachimbaji madini Tanzania (FEMATA) ametoa wito kwa wachimbaji wote yakiwemo makampuni makubwa ya uchimbaji wa madini kujitokeza kumuunga mkono Rais Dr John Magufuli katika harambee ya kuchangia madawati kwa shule mbali mbali hapa nchini. Huku akisifu mwitikio mzuri wa kampuni ya Sunshine Minning kwa kuunga kuitikia wito huo kwa kuchangia madawati 100 yenye thamani ya Tsh milioni 85,000 kwa Halmashauri ya wilaya ya Iramba mkoani Singida . Akizungumza na waandishi wa habari jana ,Rais wa FEMATA John Bina alisema kuwa Shirikisho lake limelazimika kumsaidia Rais Dr Magufuli kuhamasisha uchangiaji wa madawati kwa wanachama wake ili kumaliza kabisa tatizo hilo la uhaba wa madawati na kuona sekta ya elimu nchini inaboresheka zaidi kwa kuhakikisha wanafunzi hawakai chini. Bw Bina alisema kuwa katika kuunga mkono jitihada za serikali wao kama sehemu ya wadau wa maendeleo katika Taifa hawakupenda kuwa nyuma kujitokeza kuchangia madawati hasa ukizingatia kuwa elimu bora ni mwanzo wa kuwa na taifa bora . "Suala hili la elimu si la serikali pekee kila mmoja kwa nafasi yake ana umuhimu katika kuboresha elimu nchini na si vema kwa kila jambo kuitazama serikali ......serikali ina nafasi yake ila na sisi wadau tuna nafasi yetu katika kuiunga mkono serikali pia wanafunzi wananafasi yao .... walimu na wazazi pia " alisema rais Bina Hata hivyo aliwataka wadau wengine na wananchi mmoja mmoja kwa nafasi yake kujitokeza kuunga mkono uchangiaji wa madawati ili kumaliza kabisa kero hiyo ya uhaba wa madawati mashuleni. Alisema wao kama wadau wa maendeleo kupitia FEMATA wataendelea kuunga mkono jitihada mbali mbali zinazoendelea kufanywa na serikali ya Rais Dr Magufuli jitihada zenye lengo la kulifanya Taifa kuzidi kuwa mbele kimaendeleo. Pia alisema kwa wadau wa sekta hiyo ya madini pekee kama kila mmoja atajitolea kuchangia madawati upo uwezekano mkubwa wa zoezi hilo kukamilika mapema zaidi na kuwataka wadau wengine mbali ya wale wa madini nao kwa nafasi zao kujitolea madawati badala ya kuiachia serikali pekee. “ Ninakusudia kama Rais wa FEMATA kuwakutanisha wachimbaji wote mbali na mambo mengine tutaangalia ushiriki wetu katika masuala ya kijamii yakiwemo ya uchangiaji wa madawati” Hata hivyo mkuu wa mkoa wa Singida Bw Methew Mtigumwe mbali ya kupongeza harakati za Rais huyo wa FEMATA kwa kuunga mkono agizo la rais kwa kujitolea kuhamasisha uchangiaji wa madawati bado alisema kuwa jambo hilo ni jema na linapaswa kupongezwa zaidi. Alisema katika mkoa wa Singida kila mkuu wa wilaya ameagizwa kusimamia utekelezaji wa agizo la Rais la upungufu wa madawati katika eneo lake na kuwa mkoa umejipanga kumaliza kabisa kero hiyo ya uhaba wa madawati . MWISHO

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa