Home » » DC MBONA AWAHAMASISHA WANAWAKE MUFINDI KUGOMBEA NAFASI ZA UDIWANI,UBUNGE NA URASI‏

DC MBONA AWAHAMASISHA WANAWAKE MUFINDI KUGOMBEA NAFASI ZA UDIWANI,UBUNGE NA URASI‏

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Mkuu wa  wilaya ya  Mufindi Bi Mboni Mhita akifungua  kongamano la  Umoja wa  wanawake Tanzania (UWT) wilaya ya Mufindi leo
Mkuu  wa  wilaya ya  Mufindi Bi Mboni Mhita wa  pili  kulia akiwa na viongozi mbali mbali wa UWT mkoa na wilaya ya Mufndi na Iringa vijijini kutoka kushoto ni mwenyekiti  wa UWT mkoa Bi Zainabu Mwamwindi ,mwenyekiti wa UWT wilaya ya Mufindi Bi Marcelina Mkini katibu  wa wazazi  mkoa wa Iringa Bw  Geofrey Kavenga  na mwenyekiti  wa UWT wilaya ya Iringa vijijini Bi Shakra  Kiwanga
Washiriki  wa kongamano la UWT wilaya ya Mufindi wakimshangilia mkuu wa wilaya ya  Mufindi hayupo pichani
Mkuu  wa  wilaya ya  Mufindi mkoani Iringa Bi Mboni Mhita katikati  akiwa na mwenyekiti wa umoja  wa wanawake Tanzania (UWT)  mkoa wa Iringa Bi Zainabu Mwamwindi (kulia) na mwenyekiti wa UWT wilaya ya  Mufindi Bi Marcelina Mkini ambae ni mjumbe wa NEC Taifa  akiwakilisha wilaya ya  Mufindi  leo   wakati wa ufunguzi wa kongamano la  wanawake wa  wilaya ya Mufindi lililofanyika mjini Mafinga (picha na Francis Godwin)

Mwenyekiti  wa UWT  wilaya ya Mufindi Bi Marcelina Mosha  akimkaribisha mgeni  rasmi
Washiriki wa kongamano hilo  wakifuatilia mafunzo ya afya  na uzazi na yale ya ujasiliamali
Katibu  wa UWT Mufindi
Viongozi  wa UWT mkoa na wilaya pamoja na DC mufindi  wakifuatilia mafunzo
Mtaaluam wa afya  akitoa  semina ya afya kwa  washiriki
Mtaalam wa afya  akitoa  elimu ya matumizi  sahihi ya kondom
Mwenyekiti wa UWT wilaya ya  Iringa vijijini Bi Shakra  kiwanga akitoa  salam  zake
Na FgBlog Mufindi

MKUU  wa  wilaya ya  Mufindi mkoani  Iringa Bi Mboni Mhita amewataka   wanawake  kujitokeza kwa  wingi kugombea nafasi mbali mbali za uongozi ikiwemo nafasi ya Urais katika  uchaguzi mkuu utakaofanyika mwezi Octoba mwaka  huu

Alisema ushindi  wa  wanawake  katika nafasi mbali mbali ikiwemo  ya udiwani ,ubunge na urais ni kubwa zaidi  iwapo wanawake wenyewe watajiamini na  kuepuka na maneno ya   watu ambayo kimsingi wengi  wao wanatamani  kuona wanawake  wakiwa nyuma .

 Bi  Mboni ambae ni mjumbe wa NEC Taifa alitoa rai hiyo leo katika  ukumbi wa CCM wilaya ya Mufindi  wakati akifungua  kongamano  la  umoja wa wanawake Tanzania (UWT)   alisema  kuwa muda  ukifika  wanawake  hawana  sababu ya  kuogopa  kuingia katika nafasi mbali mbali  za uongozi na  kuwa  wale  wenye  uwezo wa kugombea udiwani ,ubunge na Urais  wajitokeze bila  katika mapambano kuogopa .

Alisema  kikubwa si wanawake  kuwatazama  wenzao  wanapoingia katika mapambano  ila ni kuona  wanawake  wanatengezeza  jeshi  moja  la mapambano ya  kumsaidia kwa nguvu  zote mwanamke mwenzao anayesimama katika  kuwania nafasi  za uongozi.


Bi Mboni  alisema vijana  pia hawana  sababu ya  kuchangamkia nafasi za  uongozi mbali mbali katika uchaguzi ujao badala ya  kuwa  nyuma na  kuwa kwa upande  wake anajivunia kuwa  mkuu wa  wilaya ya  Mufindi nafasi  ambae  pia ni mkuu wa wilaya mwenye umuri mdogo zaidi   kuliko wote nafasi aliyeteuliwa na Rais Dr Jakaya  Kikwete jambo  ambalo anampongeza Rais  kwa uteuzi huo japo  kabla ya uteuzi  huo  alikuwa ni makamu mwenyekiti  wa UVCCM Taifa .

Pia  alisema  kuwa yeye pia ni miongoni mwa  wajumbe wa NEC Taifa  wadogo  zaidi ila  pia alipata  kuchaguliwa  kuwa kiongozi  wa  vijana barani Afrika na  kuwa nafasi zote   hizo amekuwa akizipata kutokana na kuthubutu na  kutojinyanyapaa kama mwanamke.

Hivyo  alisema wakati  umefika  wa vijana na  wanawake  nchini  kutumia nafasi  ya  uchaguzi mkuu wa  mwaka  huu  kujitokeza  kuwania nafasi mbali mbali bila kuogopa .

Awali akimkaribisha mkuu  huyo  wa  wilaya kufungua kongamano hilo mwenyekiti UWT  wilaya ya  Mufindi Bi Marcelina Mkini mbali ya  kumpongeza mkuu  huyo wa wilaya ya  Mufindi kwa utendaji wake mzuri bado  alisema  kuwa  wanawake  katika  wilaya ya  Mufindi  kwa  mwaka  huu  wamejipanga kugombea nafasi zote tatu ya udiwani ,ubunge na Urais

Kuwa ushindi  wa  wanawake katika nafasi mbali mbali za uongozi utatokana na  ushirikiano mzuri  wa  wanawake wenyewe katika  kuwaunga mkono  wale  wote  wanaogombea nafasi   mbali mbali na  kuwa falisafa ya UWT Mufindi ni wanawake Kwanza .

Bi Mkini ambae ni mjumbe wa NEC Taifa  akiwakilisha  wilaya hiyo ya  Mufindi   alisema  kuwa  wanawake  wa  wilaya   hiyo ya  Mufindi wamehamasishwa  vya  kutosha   kuweza kujitokeza kugombea nafasi mbali mbali  za  uongozi na  kuwa mwitikio  wa wanawake kuanza  kuamka   kugombea nafasi  za  uongozi  ulianza  kuonekana katika uchaguzi  wa  serikali za mitaa uliofanyika mapema  hivi karibuni kwa wanawake kuonyesha ushiriki  mzuri katika mchakato huo.

Bila  kutaja  kutaja  idadi ya  wanawake  walioshinda katika uchaguzi  huo bado  alisema matokeo mazuri ya uchaguzi  wa  serikali za  mitaa ambayo yaliiwezesha  wilaya ya  Mufindi  kuongoza   kwa mkoa wa Iringa kwa CCM kushinda kwa zaidi ya aslimia 90 katika uchaguzi huo wa  serikali za mitaa ni moja kazi nzuri ya  wanawake katika ushiriki  wao katika  uchaguzi  huo.

Kwani  alisema nguvu kubwa  iliyoonyeshwa na  wanawake wa  wilaya   hiyo ni chachu ya kubadili mtazamo uliokuwepo  wa  wanawake  kuendelea  kuwa madaraja ya  kuvusha wanaume  wanaogombea hivyo mtazamo huo kwa  sasa umeanza  kupotea baada ya  wanawake  kuonyesha ushiriki  wao katika  kugombea nafasi mbali mbali za  uongozi .

Bi Mkini  alisema ushahidi  wa  nguvu ya  wanawake  katika kampeni upo wazi katika  wilaya  hiyo ya Mufindi ambayo mkuu  wa wilaya ni mwanamke ,mkurugenzi ni Mwanamke na mjumbe wa NEC Taifa ambae ni  yeye mwenyewe na kuwa nafasi hiyo  aliipata baada ya  kupambana na wanaume .



MWISHO

0 comments:

 
Powered by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa