Bango la maadhimisho ya siku ya Elimu ya watu wazima, katika kijiji cha Ikuvilo, Kata ya Luhota Wilaya ya Iringa.
Ofisa
elimu ya Watu wazima Wilaya ya Iringa Bi. Asha Hamduni akitoa taarifa
ya utekelezaji wa elimu ya watu wazima katika kijiji cha Ikuvilo Wilaya
ya Iringa.
Mgeni
rasmi wa sherehe ya elimu ya watu wazima, makamu mwenyekiti wa
Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Mh. Costantino Kihwele akikagua mabanda
ya wadau wa elimu ya watu wazima katika maadhimisho ya siku ya hiyo.
Bw.
Joachim Mgimwa (wa pili kulia) mmoja wa wageni waalikwa wa hafla ya
siku ya elimu ya watu wazima iliyofanyika katika Kijiji cha Ikuvilo
Wilaya ya Iringa.
Baadhi ya wadau wa elimu ya watu wazima wakiwa katika sherehe hiyo.
Makamu
mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Mh. Costantino Kihwele
akiwahutubia wananchi waliofika katika siku ya elimu ya watu wazima. Johachim
Mgimwa akitoa ujumbe kwa wanavikundi wa Vicoba sita wa Kata ya Luhota
waliokuwa nao wakizindua vikundi hivyo katika maadhimisho hayo ya siku
ya elimu ya watu wazima. Johachim alifika
katika hafla hiyo akimwakirisha Waziri wa fedha Dr. Willium Mgimwa
ambaye ni mbunge wa jimbo hilo la Kalenga, ambapo vikundi hivyo
vilichangiwa jumla ya shilingi Milioni 8 ya ahadi.
Wanafunzi
wa chuo cha ufundi cha Ukombozi kilichopo Nyabula katika Wilaya ya
Iringa, wakiunga mkono harakati zinazofanywa na elimu ya watu wazima,
(mwenye shati la Draft ni mkurugenzi wa chuo Bw. Deo Chengelela.
Makamu
mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Mh. Costantino Kihwele
akiwa na jopo la viongozi wa Halmashauri hiyo wakikagua mabanda ya
maonyesho katika siku ya elimu ya watu wazima.
Mkurugenzi
wa chuo cha ufundi Ukombozi Bw. Deo Chengelela akitoa taarifa ya chuo
chake kwa Mh. Kihwele katika maadhimisho hayo ya siku ya elimu ya watu
wazima.
Mh.
Kihwele akitoa maagizo kwa viongozi wa Halmashauri kuhakikisha wadau
hao wanaungwa mkono na serikali katika kuongeza ajira kwa vijana kwa
kutoa elimu ya ufundi kwa jamii.
Baadhi ya wanafunzi, mwalimu na mkurugenzi wa chuo cha Ufundi Ukombozi wakiwa katika banda lao wakionyesha baadhi tu ya bidhaa wanazotengeneza katika idara ya ufundi wa kushona.
Baadhi ya wanafunzi, mwalimu na mkurugenzi wa chuo cha Ufundi Ukombozi wakiwa katika banda lao wakionyesha baadhi tu ya bidhaa wanazotengeneza katika idara ya ufundi wa kushona.
Mh.
Kihwele akizungumza na kikundi cha akiba na mikopo cha Vicoba moja ya
vikundi sita vilivyozinduliwa katika siku hiyo ya elimu ya watu wazima.
Bw. Bonus Fivawo mkazi wa Nyabula, aliyefika katika kijiji cha Ikuvilo kuunga mkono maadhimisho ya siku ya elimu ya watu wazima.
Bw. Bonus Fivawo akionyesha moja ya mazao (Aloveira).
Bw. Bonus Fivawo akionyesha zao la Zukini (Zuchini) ambalo pia hutumiwa kama dawa.
Mmea aina ya Boga (Zuchin) unaoliwa tunda na majani yake huku ukiwa ni sehemu ya tiba.
Mkaguzi
mkuu wa shule Bi. Martha Silavwe na viongozi wengine wa Halmashauri ya
Wilaya ya Iringa, wakishangilia jambo katika siku hiyo ya elimu ya watu
wazima.
Bi. Martha Silavwe akitoa ujumbe katika hafla hiyo.
Bi. Asha Hamduni ofisa elimu ya watu wazima (Katikati) akifuatilia jambo katika sherehe hiyo ya elimu ya watu wazima.
Mzee
wa Kihehe akiwaunga mkono kikundi cha watoto 9 wa familia moja,
kinachojihusisha na Utamaduni wa ngoma ya Kihehe "Njuga au Mangala).
Mmoja
wa wazee wa kabila la Wahehe akifurahishwa na ngoma ya watoto, ya
kabila lake "Hehe" baada ya watoto hao kutia fora katika maadhimisho
hayo na kumfanya kila moja kuvutiwa nao.
Kweli
Mtoto wa Nyoka ni Nyoka, Watoto hawa wakisakata haswa ngoma ya Njuga,
ambapo kila mmoja aliyeguswa aliamua kutoficha hisia zake kwa kuinuka
na kucheza.
Naye Bw. Johachim Mgimwa hakuvumilia uhondo wa "Livangala" au Njuga
Bw. Johachim Mgimwa naye anaamua kulisakata Livangala, chezea Njuga wewe!!??.
Bila ajizi watu walimwaga fedha kwa kundi hilo la watoto, kwa kuunga mkono jitihada zao za kudumisha Mila ya Wahehe.
Mratibu
wa VICOBA Mkoa wa Iringa Bi. Tisiana Kikoti akisoma taarifa ya Vicoba
sita vya Kata ya Luhota, vikundi vyenye lengo la kuanzisha Benki ya Kata
Luhota, aliyeshika Mic (Kisemeo) ni afisa Utamaduni wa Wilaya ya
Iringa.
Viongozi
wa Vikundi sita vya Vicoba Kata ya Luhota wakiwa katika Picha ya pamoja
mara baada ya vikundi vyao kuzinduliwa rasmi na Johakimu Mgimwa
aliyemwakirisha Waziri Mgimwa ambaye ni mbunge wa jimbo hilo la Kalenga,
(mwenye suti) ni Mratibu wa Vicoba mkoa wa Iringa Bi. Tisiana Kikoti.
<<<<<<<<<<<<HABARI>>>>>>>.
JAMII
imetakiwa kuacha fikra potofu juu ya elimu ya watu wazima, kwa kuiona
elimu hiyo ni maalumu tu kwa watu wasio jua kusoma, kuandika na kuhesabu
(KKK).
Rai
hiyo imetolewa na afisa elimu ya watu wazima Wilaya ya Iringa Bi. Asha
Hamduni katika maadhimisho ya siku ya elimu ya watu wazima iliyofanyika
katika kijiji cha Ikuvilo katika Kata ya Luhota Wilaya ya Iringa.
Bi.
Hamduni amesema ipo haja kwa jamii kubadili fikra hiyo, kwani elimu
hiyo sasa inaendana na wakati na kuwa inatolewa pia kwa wanafunzi
waliohitimu elimu ya darasa la saba na kushindwa kendelea na masomo ya
elimu ya sekondari.
Aidha
Bi. Hamduni amesema awali elimu hiyo haikuwa na tija kwa baadhi ya
walengwa kutokana uwepo wa vitabu vinavyofundisha masomo ambayo
hayawafai baadhi ya wananchi wa Mikoa mingine.
Akitolea
mfano wa kitabu kilichokuwa kinafundisha kilimo cha zao la Korosho
Mtwara, Bi. Hamduni amesema vitabu hivyo havikuwa na tija kwa wananchi
wa mikoa ambayo haijihusishi na kilimo hicho na hivyo kisomo cha elimu
ya watu wazima kupuuzwa.
Pia
amesema baadhi ya changamoto zinazoikabiri idara ya elimu ya watu
wazima ni pamoja na utoro kwa watu maarufu ambao huona aibu kuhudhuria
masomo hayo, huku malipo duni (Honoralia) ya shilingi elfu 20 kwa mwezi
nayo yakichangia kuwakatisha tamaa walimu wanaotoa elimu hiyo.
Hata
hivyo amesema Wizara kupitia idara ya elimu watu wazima imebadili mfumo
wa masomo huku masomo ya masafa marefu pamoja na elimu ya ufundi stadi
ukiwahusisha watu wa elimu mbalimbali.
0 comments:
Post a Comment