Home » » WAIGIZAJI KUPEWA MAFUNZO MKOANI IRINGA!

WAIGIZAJI KUPEWA MAFUNZO MKOANI IRINGA!

Mdhamini mkuu wa mafunzo ya Uigizaji na utayarishaji wa Filamu kwa wasanii wa mkoa wa Iringa kwa kushirikiana na asasi ya TCDA na shirikisho la filamu Tanzania (TAFF) Fredrick Mwakalebela.
=====  =====  ======
WAIGIZAJI KUPEWA MAFUNZO

Na Denis Mlowe,Iringa

SHIRIKISHO la Filamu Tanzania(TAFF) kwa kushirikiana na asasi isiyo ya Kiserikali ya Tanganyika Centre For Development and Advocacy (TCDA) wameandaa mafunzo ya uigizaji na utayarishaj wa filamu kwa wasaniin wa mkoa wa Iringa na maeneo ya jirani.


Akizungumza na Daraja letu mkurugenzi wa asasi hiyo, Jackson Kiyeyeu alisema lengo la mafunzo hayo ni kuwapa upeo na ujuzi zaidi wasanii wa Iringa katika kuweza kuandaa filamu bora na kuwa na ujuzi wa katika uigizaji.


Alisema mafunzo hayo yatakuwa ya mwezi mmoja na yatatolewa na wasanii wakali wa filamu Tanzania akiwemo msanii nguli  Haji Adam maarufu kama Baba Haji akiambatana na walimu wa sanaa kutoka Dar es Salaam.

Kiyeyeu alisema wahitimu wa mafunzo hayo watapatiwa vyeti vinavyotambulikana shirikisho la filamu Tanzania na wasanii bora 10 watapatiwa fursa ya kushiriki filamu ya No Option itakayochezwa na wakali wa Bongo Movie.

“ Mafunzo yatatolewa kwa watu wote kuanzia elimu ya shule ya msingi hadi kidato cha sita na vyeti vitakavyotolewa vitawawezesha kufanya kazi za filamu popote pale Tanzania na ni wakati wa wasanii sasa kuwa na elimu ya ugizaji na utayarishaji wa filamu kuliko ilivyo sasa wengi wao kutokuwa na elimu.” Alisema Kiyeyeu

Mafunzo ya ugizaji na utayarishaji wa filamu yatakakuwa ni mara ya kwanza kwa mkoa wa Iringa yamedhaminiwa na aliyekuwa katibu mkuu wa TFF Fredrick Mwakalebela aliyetoa asilimia 75 ya ada za mafunzo hayo kwa wasanii wa Iringa.


Kwa upande wake Daraja Letu lilipozungumza na Mwakalebela alisema  lengo ni kuwasaidia wasanii wa Iringa kuweza kuwa na ufahamu wa uigizaji na utayarishaji wa filamu bora Tanzania na kuwakomboa vijana katika umaskini.

Alisema sanaa ya uigizaji wa filamu una faida kubwa sana katika kuondokana na tatizo la ajira kwa vijana natoa wito wajitokeze kwa wingi na kuwataka wadau kuweza kuwasaidia vijana katika kuondokana na tatizo la umasikini katika kuwaidia kutimiza ndoto zao.

“Kutokana na kupenda sanaa  na michezo kwa ujumla ameguswa sana na wazo la TCDA kuweza kunipa mawazo yao hivyo sikuwa na budi kuweza kuwadhamini katika hilo nachoomba wadau wengine waweze kujitokeza kuwasaidia wasanii wa Iringa kuweza kutambulika kitaifa na kimataifa katika tasnia ya Filamu.” Alisema Mwakalebela

Alisema Iringa kuna wasanii wengi wanaojitahidi kupambana kwa uwezo wao binafsi kufanya sanaa kwa kile anachofikiria bila elimu ya sanaa ya ugizaji na utayarishaji wa filamu.

Mwakalebela alisema wasanii watakaofanya vizuri katika mafunzo hayo watashirkishwa katika filamu mbalimbali ambazo zinaandaliwa na wasanii wakubwa kutoka jiji Dar es salaam kwa lengo la kuwainua mbeleni waweze kujitegemea.

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa