KATIKA
kukabiliana na changamoto za sekta ya elimu mfuko wa Pensheni kwa watumishi wa
Umma -PSPF umekabidhi mabati 100 pamoja na mifuko ya saruji 150 vifaa vyenye thamani
zaidi ya shilingi Milioni 2. 5 kwa shule ya sekondari Mlowa iliyopo katika
halmashauri ya Wilaya ya Iringa.
Akikabidhi
msaada huo meneja wa PSPF Msafiri Mugaka amesema hatua hiyo imekuja baada ya
kutambua uwepo wa changamoto mbalimbali katika shule hiyo na wao kama jamii
kuamua kuisaidia shule hiyo.
Aidha
Mugaka amesema shule hiyo imekuwa na matatizo ya majengo na hivyo PSPS kama
walezi na waandaaji wa watumishi wa kesho wameona ni vyema kushiriki kikamilifu
katika kutatua tatizo hilo.
Akipokea
msaada huo Kaimu mkuu wa Wilaya ya Iringa Gerlad Guninita amesema msada huo wa
PSPF ni mkubwa kwani umewasaidia wanafunzi kuwaepusha na hali ya kukosa mabweni
na hivyo kuwafanya kukosa muda wa kutosha wa kujisomea.
Shule
ya sekondari Mlowa inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ya wanafunzi
kulala katika sakafu ya vyumba vya madarasa hali itokanayo na kukosekana kwa
mabweni na vitanda.
0 comments:
Post a Comment