Home » » DC Kilolo apiga marufuku magari ya halimashauri kuwapeleka maofisa katika matanuzi Iringa Mjini, atishiwa kuuawa, aomba ulinzi

DC Kilolo apiga marufuku magari ya halimashauri kuwapeleka maofisa katika matanuzi Iringa Mjini, atishiwa kuuawa, aomba ulinzi

MKUU wa Wilaya ya Kilolo Mkoani Iringa Mh. Gerlad Guninita ameomba kupatiwa ulinzi madhubuti, baada ya kupokea vitisho vinavyoashiria hatari ya uhai wake, hatua inayotokana na kuwaadabisha kwa kudhibiti mienendo mibovu ya baadhi ya watumishi wa Halmashauri hiyo ya kilolo ambao wamekuwa wakikaidi kutekeleza majukumu yao.

Akizungumzia wasiwasi wa hatari hiyo katika kikao cha baraza la madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo mkoni Iringa, Guninita amesema amekuwa akipata vitisho baada ya kutoa adhabu kwa watumishi mbalimbali wilayani humo huku baadhi yao wakidiliki kumtumia njia ya ujumbe wa Simu, hatua inayoashiria maisha yake kuwa hatarini, jambo linalosababisha kuishi kwa mashaka na kulazimika kufungua jalada polisi lenye namba IR/RB/1799/2013 katika kituo cha Polisi Iringa. 

Guninita amesema baadhi ya watumishi wamemchukia zaidi baada ya kubana njia za ubadhilifu wa fedha za umma, na kupinga utaratibu wa baadhi ya watumishi kuishi Iringa mjini umbali wa zaidi ya km 40 na kusababisha kuchelewa kufika kazini huku kukiwa na matumizi holela ya magari na mafuta, kwa kuwa watumishi hao hupelekwa Kilolo na kurudishwa tena Iringa mjini, jambo linalochangia ufujaji mkubwa wa fedha za wananchi, fedha ambazo zingefanya shughuli za kiuchumi. zaidi msikie hapa

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa