Home » » WAPINGA TAMKO LA SERIKALI LOLIONDO

WAPINGA TAMKO LA SERIKALI LOLIONDO

HATIMAYE wanafunzi wa jamii ya wafugaji, wanaosoma katika vyuo vikuu mkoani Iringa, wameungana na kutoa tamko juu ya mgogolo wa Loliondo mkoani Arusha, huku wakimtaka waziri mwenye dhamana ya maliasiri na Utalii, Barozi Hamis Kagasheki huku kurejea upya namna ya kutatua mgogolo huo.

Tamko hilo limetolewa na umoja wa wanafunzi wa vyuo vikuu wanaotoka katika jamii ya wafugaji, na akisoma  tamko la wanachuo hao Solomon Lekui amesema kamwe wao hawapo tayari kushuhudia wazazi wao wakipokonywa ardhi ambayo ni mali yao halali.

Lekui amesema serikali inapaswa itafakari zaidi suala la wafugaji kitaifa, kwa kuunda  Tume maalumu ya kukusanya maoni ya wafugaji kote nchini katika kutafuta namna ya kutatua kikamilifu migogolo, kwa kuwashirikisha wafugaji wenyewe  ili wapate fulsa ya kubainisha changamoto na matatizo yanayowakabiri.

Emmanuel Ole Kileli mwanafunzi kutoka chuo kikuu cha Tumaini amesema imekuwa kama desturi kwa wafugaji kulalamika mambo mbalimbali yanayohusiana na unyang’anyi wa ardhi yao inayoambatana na uhamishaji kwa kutumia nguvu na upotevu mkubwa wa mali na maisha yao.

amesema Serikali imekuwa mstari wa mbele katika kutekeleza maamuzi magumu kwa wafugaji nchini, kwa madai kuwa wafugaji wanakiuka sheria kwa kuvamia maeneo mbalimbali yasiyo ya ufugaji hasa maeneo ya hifadhi naya kilimo, na kuwa hatua hiyo ni kutokana na kukosekana kwa sera ya ufugaji asili (Pastoralism Policy) ambayo ingehusika kuratibu na kuthamini shughuli mbalimbali za ufugajiasili na mazao yake kwa ujumla.Wamesema serikali itambue wafugaji nao wanayo haki kama walivyo watanzania wengine, na sasa kuna haja ya kutoa vipaumbele sawa kwa kundi la wakulima na wafugaji.

Saikoni Justin  mwenyekiti wa umoja wa wanachuo wanatoka katika jamii ya wafugaji, amesema kuna ukiukwaji wa sheria za kimataifa katika uchukuaji wa ardhi ya Loliondo na wao kama wamesomeshwa na mifugo na wanayo haki ya kutetea jamii yao, huku akiitaka  serikali kuacha Propaganda ambazo hazina maslahi wala tija kwa wananchi wake, na badala yake itumike busara katika utatuzi wa migogolo pasipo kuingiza masuala ya Siasa.

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa