Home » » TUEPUKANE NA VYAMA VYA SIASA VINAVYOHAMASISHA VURUGU ASEMA MSAMBATAVANGU

TUEPUKANE NA VYAMA VYA SIASA VINAVYOHAMASISHA VURUGU ASEMA MSAMBATAVANGU




 Bi.Jesca Msambatavangu mwenyekiti  wa CCM mkoa wa Iringa

MWENYEKITI  wa  chama  cha mapinduzi (CCM) mkoa  wa Iringa  Jesca Msambatavangu  amempongeza Rais Dkt Jakaya  Kikwete  kwa  kuendelea kudumisha amani ya taifa na kuwataka a  wana CCM mkoani Iringa  na nchini kote kuendelea  kudumisha amani na mshikamano na kuepukana na siasa vya vurugu ili kuendelea kumuunga mkono Rais Dkt Kikwete na kumuenzi hayati baba  wa Taifa  Mwalimu Julius Nyerere katika  kudumisha amani  ya Taifa letu.

 Akiwahotubia  wana CCM  wa tawi la Mkwajuni  kata ya Nyanzwa  tarafa ya Mahenge  wilaya ya  Kilolo  mkoani Iringa jana  katika maadhimisho ya miaka 36 ya  kuzaliwa kwa  CCM,Msambatavangu alisema kuwa  kuanzishwa  kwa mfumo  wa  vyama  vingi  kulilenga kukuza demokrasia nchini  ila  sasa vyama vya  siasa  hasa vyama  vya upinzani  vimegeuza siasa ni ulingo  wa matusi na vurugu jambo mbalo ni kinyume na malengo  sahihi  ya kuanzishwa  kwa  mfumo  huo  wa  vyama vingi  nchini.



Hivyo  alisema  ni heri  kubaki na chama  kimoja ambacho  kimelifikisha hapa  lilipo bila  watu  kugombana  wala  kumwaga  damu badala ya  kuendelea  kutaka  kuwa na serikali ya vyama  ambavyo vimeshindwa  kulinda amani  yetu na  kuendelea  kulichafua Taifa kwa vurugu aza kisiasa  zisizo na ukomo jambo ambalo ni hatari kama  litaendelea  kupewa nafasi katika jamii yetu



Msambatavangu  alisema vyama  vya  upinzani  vimekuwa ni chanzo cha kuanzisha  fujo katika mikutano ya CCM na kuwa  kutokana na mbinu hizo chafu hivi  sasa CCM imejikita zaidi katika  kuwaeleza  wananchi utekelezaji  wa ilani yake badala ya  kuanza  utekelezaji  wa ajenda za baadhi ya  vyama  vya  siasa ambavyo wakati  wote kwao  vurugu ni kama mtaji  wa kisiasa.



Hata  hivyo  mwenyekiti  huyo  wa CCM mkoa  wa  Iringa aliwataka  wana CCM kuendelea  kuendesha siasa kwa kuzingatia amani ya Taifa na kila wanapotimiza  wajibu  wao kujaribu  kujikumbusha misingi  ya amani na utulivu iliyoachwa  na  mwalimu Nyerere na  jitihada zinazoendelezwa na mwenyekiti  wa CCM  Taifa Dkt  Rais    Kikwete  katika  kudumisha amani ya Taifa  letu.



Alisema  kuwa  mwenyekiti  wa CCM Dkt Kikwete amekuwa ni kiongozi  wa mfano kwa  Taifa  katika kuliongoza Taifa  kwa misingi ya baba wa  Taifa  hayati Nyerere na kuwa wakati wote Dkt Kikwete  amekuwa  akikemea vitendo vya uchochezi na uvunjifu  wa amani ya Taifa  vinavyofanywa na baadhi ya  viongozi  wa vyama  vya kiasia hapa nchini .


Alisema  kuwa  kila mtanzania anayo nafasi ya  kumsaidia  Rais Kikwete katika  kupigania amani ya Taifa  na kujiepusha na vyama vya siasa ambavyo vipo kwa ajili ya kuvuruga amani ya Taifa na kuwa iwapo Taifa litakosa amani na utulivu si wana CCM peke yao ambao watayakimbia makazi yao ila ni wananchi  wote wataishi maisha ya kuhangaika kama ilivyo leo Somaria na Ethiopia ambako Raia wake  kila  kukicha  wanayakimbia makazi yao.

"Ndugu  zangu kama  tumefanikiwa  kufika hapa  tulipo leo kwa CCM kuadhimisha  miaka 36 bila kumwaga damu na tumeruhusi mfomo  wa vyama  vingi ambavyo vinaendelea  kuchochea vurugu ....kuna haja gani ya  kujiunga na vyama visivyopanda amani na kuachana na CCM  kilichoweza kulinda amani.....nawaombeni tusiyumbishwe na bendera  za vyama  tuendelee kubaki CCM" alisema Msambatavangu

Akielezea  kuhusu CCM ilivyoendelea  kutekeleza ilani  yake katika sekta ya  Kilimo alisema  kuwa  Kilimo  ni  moja kati ya  sekta tegemeo kubwa  kwa uchumi wa Taifa  hivyo lengo ni kujenga Uchumi wa kisasa  utakaopelekea  Taifa letu kujitegemea.



"Sasa kama wengine wanazalisha mbegu bora, wauzaji wanachakachuka, wakulima wanapewa mbegu na mbolea za ruzuku wanauza vocha, Vyuoni hakuna utafiti wakutosha kusaidia mapinduzi haya ya kilimo ni tatizo katika kufikia mpango wa maendeleo wa Taifa letu"

Alisema  hivyo Serikali ya  CCM kupitia  Ilani yake ya mwaka 2010-2015 inalengo la Kuongeza KASI ya ujenzi wa Uchumi wa Kisasa na Taifa linalojitegemea kwa kuwashirikisha na kuwawezesha kiuchumi wananchi.

Msambatavangu  alisema katika  kufikia malengo hayo ya  Kuongeza maarifa na matumizi ya sayansi na Teknolojia katika sekta za Uzalishaji wakulima  wameendelea  kusaidiwa mbinu na pembejeo za  ruzuku Ili kuongeza Uzalishaji,Ufanisi na Tija au faida katika uchumi hususani katika     Kilimo  .
Na Francis Godwin

0 comments:

 
Powered by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa