na Amana Nyembo, Iringa
WAKULIMA mkoani
Iringa wameondolewa wasiwasi wa kutumia mbolea ya Minjingu itakayokuwepo kwenye
pembejeo za ruzuku msimu ujao kwa kuelezwa kuwa imeongezwa virutubisho, hivyo
haina madhara kwa matumizi.
Awali wakulima
walikuwa na hofu ya kutumia mbolea hiyo kutokama na mbolea hiyo iliyokuwa
imegawiwa na serikali, kusababisha mavuno hafifu.
Akizungumza na
wakulima hao hivi karibuni kwa nyakati tofauti katika vijiji vya Mbigili na
Lulanzi mbele ya wanahabari waliokuwa ziarani mkoani Iringa kwa ufadhili wa
Baraza la Kilimo Tanzania (ACT), Ofisa Mazao na Pembejeo Wilaya ya Kilolo,
Watson Matamwa, alisema Minjigu ni mbolea ya vumbi ni nzuri katika kilimo.
Alisema msimu
uliopita mbolea hiyo ililetwa mapema bila maelekezo yoyote, lakini kwa sasa
imefanyiwa kazi na wale walioitumia msimu uliopita na kupata mavuno kidogo
msimu ujayo watapata mavuno mengi kutokana na mbolea, hivyo kudumu muda mrefu
ardhini.
“Minjingu ni
mbolea inayoweza kupambana na tindikali, haiharibu udongo, ni mbolea ya asili
na ukiweka shambani mavuno yako yataendelea kuwa mazuri kwa miaka miwili hadi
mitatu,” alifafanua Matamwa na kusema sasa imeongezwa virutubisho.
Awali akizungumzia
mbolea hiyo, mkulima Yeteri Kiongosi kutoka Kijiji cha Lulanzi alisema mbolea
hiyo walipoitumia haitoa tija yeyote katika kilimo cha mahindi.
Mpagama
alisema: “Baada ya kupata mavuno kidogo, tulifanya majaribio katika mazao yote
tukaona Minjingu inafaa katika zao la tumbaku na pareto.”
Chanzo: Tanzania Daima
0 comments:
Post a Comment