Hili ni jiwe Igeleke ambalo ni sehemu ya utalii katika Manispaa ya Iringa ,isiyopewa kipaumbele na ofisi ya utalii
Hapa ukiwa juu ya jiwe hilo unaweza kutazama maeneo mbali mbali ya mji wa Iringa mbele kule ni sehemu ya uwanja wa ndege Nduli
Wageni kutoka nje ya Tanzania hupenda kutembelea eneo hili bila malipo kutokana na uongozi wa Manispaa ya Iringa kutoweka mkakati wa kutumia jiwe hili kutangaza utalii wa ndani
Ni eneo linalovutia zaidi ukiwa barabara kuu ya kuelekea uwanja wa Ndege nduli
Hapa ni chini ya jiwe Igeleke kunapendeza sana
Picha na Francis Godwin
0 comments:
Post a Comment