Mkuu wa Wilaya ya
Iringa Richard Kasesera amesema katika utumishi wake kwa wananchi hana mbwembwe
kama baadhi ya watu wanavyodai bali anafanya kutokana na hali halisi na eneo
husika.
Kasesera ameyasema hayo
alipokuwa akizungumza katika kipindi cha HOTMIX kinachorushwa na EATV, ambapo
ameweka wazi kwamba anafanya kazi yake ya kuwatumikia wananchi na ofisini
hushinda mara chache sana ili kuonana na wananchi na kutatua kero zao katika maeneo
yao.
“Mimi sina mbwembwe,
mfano zile picha zinazoonyesha nikiwa kwenye maji nikiokoa watoto, kule mvua
ilinyesha kitongoji kizima kikawa kinatakiwa kuokolewa ikabidi niende na
viongozi wenzangu kufanya uokozi na Mungu alisaidia tukafanya vyema” Amesema
Kasesera
Aidha Kasesera
ameongeza kuwa baada ya kuteuliwa kwa mara ya kwanza na Rais Mstaafu Dkt.
Jakaya Kikwete aliingia kazini moja kwa moj a hivyo hakuwahi kupata semina ya
ukuu wa wilaya, na alipoteuliwa na Rais Dkt. John Magufuli akawa tayari amepata
uzoefu wa kuendelea kutumikia umma.
Pamoja na hayo DC
Kasesera amewataka viongozi wa umma kutumia mitandao ya kijamii kwani imekuwa
ikitoa taarifa mbalimbali kuhusu kero za
wananchi.
‘Mimi natumia mitandao
ya kijamii mingi, hasa facebook imekuwa ikinisaidia sana ambapo watu hunitumia
ujumbe mfupi ‘meseji’ na nikifuatilia mambo hayo hukuta ni kweli na kuyatatua
kwa haraka.
Wakati huo huo DC
Kasesera amesema hana ugomvi na viongozi wa UKAWA katika wilaya yake na
anafanya nao kazi kwa ushirikiano kwani anatekeleza kwa vitendo falsafa ya
‘hapa kazi tu’.
0 comments:
Post a Comment