Kushoto
kwenda kulia ni Afisa Utalii Nyanda za Juu Kusini Gervas Mwashimaha,
Ofisa Utalii wa Tanapa wa ofisi ya Utalii Kanda ya Nyanda za Juu Kusini
Risala Kabongo, Kaimu Meneja Masoko TANAPA Victor Ketansi na Afisa
Mawasiliano Mwandamizi TANAPA Catherine Mbena wakiongea na wanahabari
mkoani Iringa jana. (Picha na Friday Simbaya).
SHIRIKA
la Hifadhi za Taifa (TANAPA) kupitia hifadhi zake 16 linakusudia
kukusanya zaidi ya 2.5bn/- katika kampeni ya kuhamasisha watu kutembelea
hifadhi za taifa ili kuhamasisha utalii wa ndani, yeney kauli mbiu
yake, “Tembelea Hifadhi Uzawadike.”
Kaimu
Meneja Masoko TANAPA, Victor Ketansi akiongea na waandishi mkoani
Iringa jana iliweka msisitizo katika kutangaza na kuhamasisha utalii wa
ndani ili kupunguza utegemezi kwa watalii wa kigeni.
Alisema
kuwa TANAPA kwa kushirikiana na makala wa utalii (tour operators)katika
kampeni hiyo ya miezi sita (6) iliyoanza Julai 1 hadi Desemba 31, 2015
watanzania watumia fursa hii kutembelea Hifadhi za Taifa na kujipatie
zawadi kemkem katika kipindi hiki cha kampeni.
Alisema
kwa pamoja na kwamba utaburudika, kushangaa na kufurahia kuona vivutio
mbalimbali, pia utapata zawadi mbalimbali zitakazotolewa kwa kila
atakayetembelea hifadhi wakati huu wa uhamasishaji.
“Washirika/wadau
wetu wapo katika mikoa ya Mwanza, Dar es Salaam, Arusha, Kilimanjaro,
Iringa, Morogoro na Mbeya mjini,” alisema kaimu meneja masoko wa TANAPA.
Zawadi
zitakazotolewa ni DVD za wanyama,Vitabu vya wanyama, Tshirts, Kofia,
Tai za TANAPA, zawadi nono ya kwenda kutalii katika Hifadhi ya Taifa
Serengeti au Gombe kwa muda wa siku TATU na kulala katika hotel yenye
hadhi ya Nyota tano.
Hata
hivyo, Kaimu Meneja Masoko TANAPA, Victor Ketansi alisema kuwa tangu
kuanzisha kwa kampeni za kuhamasisha jamii tembelea hifadhi za taifa
utalii wa ndani umeomgezeka ambapo kwa mwaka watalii 427,208 alitembea
hifadhi za taifa.
Kwa Hifadhi ya Saanane na Kilimanjaro zawadi itatolewa kwa taasisi itakayopeleka idadi kubwa ya watalii.
Kampeni hii na zawadi husika haziwahusu wafanyakazi katika kampuni za kitalii na mahoteli yaliyoko ndani na hifadhi.
Mchanganuo wa Zawadi zitakazotolewa.
Katika
kipindi hiki cha kampeni kwa yeyote atakayetembelea hifadhi zaidi ya
mara moja atapata zawadi isipokuwa kwa hifadhi za Taifa Saanane na
Kilimanjaro (Hizi zina zawadi kwa utaratibu tofauti).
Ukitembelea hifadhi ya Taifa yoyote zaidi ya mara moja utajipatia DVD yenye wanyama mbalimbali.
Ukitembelea hifadhi ya Taifa yoyote zaidi ya mara mbili utapata DVD ya wanyama na fulana ya TANAPA, Kofia au Tai.
Ukitembelea
hifadhi ya Taifa yoyote zaidi ya mara tatu utajipatia DVD yenye wanyama
mbalimbali, fulana, Kofia, Tai na Kitabu cha wanyama.
Ukitembelea
hifadhi zaidi ya mara nne utapata zawadi zote hapo juu pamoja na zawadi
ya juu kabisa ambapo, utapelekwa kutalii katika Hifadhi ya Taifa
Serengeti au Gombe (kuangalia sokwe) na kulala katika hotel yenye hadhi
ya nyota tano kwa muda wa siku TATU kwa gharama za TANAPA.
Kwa
hifadhi za Kilimanjaro na Saanane: Itazawadiwa taasisi au mtu itakayo
peleka wageni wengi zaidi kipindi cha kampeni hii Julai- Disemba, 2015.
Saanane-Mtu atakayepeleka watalii wasiopungua 1500 atapewa zawadi ya juu kabisa
Kilimanjaro -Taasisi itakayopeleka watalii wasiopungua 150 kwa kipindi chote cha kampeni itajipatia zawadi ya juu kabisa.
MUDA WA KAMPENI
Kampeni hii itakuwa ya miezi sita (6). Kuanzia Julai 1 hadi Disemba 31, 2015
VITUO VYA KUJIANDIKISHA NA KULIPIA
Vituo
vipo mikoa ya Dar es Salaam, Arusha, Kilimanjaro, Mwanza, Iringa,
Morogoro na Mbeya Wadau wa utalii wote (tour operators) wanakaribishwa
kushiriki.
Muhimu kwa watalii wetu:
Kujiandikisha jina na namba ya kitambulisho cha aina moja kila aingiapo hifadhini ili tumtambue kwa ajili ya zawadi.
Wenye
usafiri binafsi wanaweza tembelea hifadhi bila kupitia vituo
vilivyotajwa hapo juu.Wazingatie kujiandikisha katika kitabu maalum
kilichopo katika lango la kuingilia hifadhini.
Huduma
za malazi ya bei nafuu ndani ya hifadhi zinapatikana. Vituo vyetu
vilivyotajwa hapo juu vitatoa taarifa zote kwa aina ya utalii wowote
unaohitaji ndani ya hifadhi.
Sheria
na taratibu za hifadhi ziendelee kuzingatiwa wa kutoa elimu ya uhifadhi
ili kuhakikisha jamii inanufaika na shughuli za uhifadhi katika maeneo
yanayozunguka hifadhi.
0 comments:
Post a Comment