Mbunge Mgimwa akimkabidhi madawati diwani wa kata ya Mgama Bw Lupala |
Mbunge Mgimwa akikabidhi madawati 30 kwa viongozi wa serikali ya kijiji cha Lwato kata ya Mgama |
Mbunge Mgimwa akisalimiana na wananchi wa kata ya Mgama |
Mzee mkazi wa Mgama akimweleza jambo mbunge Mgimwa |
Mbunge wa jimbo la Kalenga Godfrey Mgimwa kulia akisaidiana na diwani wa kata ya Mgama Bw Denis Lupala kushusha madawati katika lori kwa ajili ya shule ya msingi Lwato |
Mbunge wa jimbo la kalenga akiwa katika usafiri wa Baiskeli kuelekea katika kukagua miradi ya maendeleo kata ya Mgama |
Mbunge wa Kalenga wa tatu kulia akiwa na wadau wa maendeleo kata ya Mgama |
Wananchi wa Mgama wakiwa katika mkutano wa hadhara wa mbunge Mgimwa |
Wananchi wa Mgama wakizuia msafara wa mbunge Mgimwa kwa furaha ya kupelekeza umeme |
Mbunge wa jimbo la Kalenga Godfrey Mgimwa amekabidhi madawati 30 kwa shule ya msingi Lwato kata ya Mgama huku akiwataka wananchi kutodanganyika na wanaojipitisha Kwani bado anautaka ubunge tena ila kuzidi kuwatumikia.
Akizungumza na wakazi wa vijiji vya kata ya Mgama kwa nyakati tofauti jana baada ya kukabidhi msaada wa madawati kwa shule ya mpya ya msingi ya Lwato kama sehemu ya utekelezaji wa ahadi yake ,mbunge Mgimwa alisema bado anautamani ubunge hadi hapo dhamira yake ya kimaendeleo itakapo timia.
Hivyo alisema lengo lake ni kuhakikisha anatekeleza ahadi zote zilizoachwa na mbunge aliyetangulia mbele za haki Dr Wiliam Mgimwa kabla ya muda wa kuvunja bunge kufika na kuwa kwa sehemu kubwa tayari ahadi hizo amezitekeleza .
Alisema kuwa amepata kutekeleza ahadi mbali mbali zilizoachwa na mbunge aliyetangulia katika jimbo hilo la Kalenga kwa kipindi kifupi zaidi kutokana na kuwa na moyo wa kuwatumikia wananchi wa jimbo hilo la Kalenga kwa kipindi kijacho baada ya uchaguzi mkuu wa Octoba mwaka huu.
" Wapo baadhi ya watu wanajipitisha pitisha na kudanganya wananchi kwa kuwahonga pesa kwa madai kuwa mimi sitagombea ubunge tena wa kalenga ......leo nawahakikishieni kuwa mimi nitagombea tena ubunge mwaka huu ili niweze kuwatumikia zaidi baada ya huu ubunge wangu wa mwaka mmoja kumalizika .......umri wangu bado unaruhusu kuendelea kuwatumikia hadi vipindi vinne ama zaidi mimi bado kijana na pia nimesoma najitambua zaidi .....wanaowatenga kwa kuwahonga wachache pesa wacha waendelee ila mimi nitahakikisha naendelea kuwaletea maendeleo wananchi wote bila kujali itikadi za vyama vyetu"
Awataka kutoacha kupokea pesa za wagombea wanaojipitisha ila
msimamo wao ni kumchagua mbunge wa maendeleo badala ya mgombea mwekezaji
ambae anagawa pesa na riba yake kuichukua Baada ya kuwa mbunge
Mbali ya kuchangia madawati hayo pia mbunge huyo amechangia kiasi cha Tsh Milioni 36 kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa maabara katika shule mbali mbali za sekondari jimbo la Kalenga huku jumla ya zaidi ya Tsh milioni 500 zikitumika katika miradi mbali mbali ya kimaendeleo katika jimbo hilo toka alipoingia madarakani mwaka jana.
Aliyataja baadhi ya maeneo ambayo amekuwa akisaidia kuwa ni pamoja na uendelezaji wa ahadi za mbunge aliyetangulia kwa kuwawezesha wananchi kufungua VICOBA zaidi na kuwa toka amekuwa mbunge jumla ya vikundi vya VICOBA 30 amevianzisha na kuviunga mkono kwa kuchangia fedha .
Kwa upande wake diwani wa kata ya Mgama Bw Denis Lupala akishukuru kazi za mbunge huyo alisema kuwa jimbo la Kalenga halina sababu ya kuendelea kubadili wabunge kama nguo na kuwa kwa muda mfupi ambao Bw Mgimwa amepata kuwa mbunge wa jimbo hilo kasi ya maendeleo imekuwa ni kubwa zaidi.
Lupala ambae pia ni katibu wa itikadi na uenezi wa wilaya ya Iringa vijijini alisema atahakikisha anashawishi wananchi wa Kalenga ili muda ukifika kwa kauli mmoja kumpitisha tena Mgimwa kuwa mgombea pekee wa jimbo hilo kutokana na kipimo cha utendaji kazi alichokionyesha kwa muda mfupi wa majaribio kwake .
Alisema moja kati ya ahadi yake kubwa katika kata yake ya Mgama ilikuwa ni umeme na tayari hadi sasa ahadi hiyo imetekelezeka kwa nguzo za umeme na nyaya kusambazwa katika eneo hilo la Mgama pia madawati katika shule ya msingi Lwato ametekeleza na shughuli nyingine nyingi .
Akizungumza kwa niaba ya wananchi wa kata hiyo ya Mgama Bw Obadia Sanga alisema kwa wananchi wa Kalenga kwa sasa wamekua na hawapo tayari kuendelea kulifanya jimbo hilo kuwa la watu kujifunzia ubunge ama kuwafanya wananchi ni mtaji wao wa kiuchumi hivyo kwa mwaka huu hawataki michepuko wataendelea kubaki njia kuu kwa kuwa na mbunge huyo tena ili kuendeleza jimbo la Kalenga.
Alisema wapo baadhi ya watu wanapita na kutengeneza matabaka katika jimbo hilo la Kalenga kwa kuwatumia wachache kuwapa pesa ili kuwashawishi wananchi na mbaya zaidi wamekuwa wakiponda kazi kubwa inayofanywa na mbunge wa CCM huku na wao ni wana CCM jambo ambalo ni hatari zaidi kwa uhai wa CCM iwapo mwana CCM badala ya kupongeza utekelezaji wa ilani ya CCM anaishia kuponda wakati wao wapinzani wamekuwa wakipongeza kazi hizo zinazofanywa na Mgimwa .
Aliyataja baadhi ya maeneo ambayo amekuwa akisaidia kuwa ni pamoja na uendelezaji wa ahadi za mbunge aliyetangulia kwa kuwawezesha wananchi kufungua VICOBA zaidi na kuwa toka amekuwa mbunge jumla ya vikundi vya VICOBA 30 amevianzisha na kuviunga mkono kwa kuchangia fedha .
Kwa upande wake diwani wa kata ya Mgama Bw Denis Lupala akishukuru kazi za mbunge huyo alisema kuwa jimbo la Kalenga halina sababu ya kuendelea kubadili wabunge kama nguo na kuwa kwa muda mfupi ambao Bw Mgimwa amepata kuwa mbunge wa jimbo hilo kasi ya maendeleo imekuwa ni kubwa zaidi.
Lupala ambae pia ni katibu wa itikadi na uenezi wa wilaya ya Iringa vijijini alisema atahakikisha anashawishi wananchi wa Kalenga ili muda ukifika kwa kauli mmoja kumpitisha tena Mgimwa kuwa mgombea pekee wa jimbo hilo kutokana na kipimo cha utendaji kazi alichokionyesha kwa muda mfupi wa majaribio kwake .
Alisema moja kati ya ahadi yake kubwa katika kata yake ya Mgama ilikuwa ni umeme na tayari hadi sasa ahadi hiyo imetekelezeka kwa nguzo za umeme na nyaya kusambazwa katika eneo hilo la Mgama pia madawati katika shule ya msingi Lwato ametekeleza na shughuli nyingine nyingi .
Akizungumza kwa niaba ya wananchi wa kata hiyo ya Mgama Bw Obadia Sanga alisema kwa wananchi wa Kalenga kwa sasa wamekua na hawapo tayari kuendelea kulifanya jimbo hilo kuwa la watu kujifunzia ubunge ama kuwafanya wananchi ni mtaji wao wa kiuchumi hivyo kwa mwaka huu hawataki michepuko wataendelea kubaki njia kuu kwa kuwa na mbunge huyo tena ili kuendeleza jimbo la Kalenga.
Alisema wapo baadhi ya watu wanapita na kutengeneza matabaka katika jimbo hilo la Kalenga kwa kuwatumia wachache kuwapa pesa ili kuwashawishi wananchi na mbaya zaidi wamekuwa wakiponda kazi kubwa inayofanywa na mbunge wa CCM huku na wao ni wana CCM jambo ambalo ni hatari zaidi kwa uhai wa CCM iwapo mwana CCM badala ya kupongeza utekelezaji wa ilani ya CCM anaishia kuponda wakati wao wapinzani wamekuwa wakipongeza kazi hizo zinazofanywa na Mgimwa .
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment