Home » » WANAWAKE WAHIMIZWA KUNYNYESHA WATOTO

WANAWAKE WAHIMIZWA KUNYNYESHA WATOTO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
WANAWAKE nchini wamehamasishwa kuwanyonyesha maziwa ya mama pekee watoto wachanga katika saa moja mara baada ya kujifungua hadi miezi sita bila kuwapa kitu chochote ikiwemo maji na juisi kwa kuwa maziwa yanachangia kwa kiasi kikubwa kuimarisha maendeleo ya uhai wa mtoto.
Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dk. Christine Ishengoma wakati wa uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji duniani kwa wanahabari na kufanyika ukumbi wa Gentle Hill na kitaifa kufanyika Wilaya ya Mufindi, Katibu Tawala Mkoa, Wamoja Ayubu, alisema wanahabari wanatakiwa kutumia kalamu zao kuhamasisha jamii kuhusu njia bora za kumsaidia mama ili aweze kunyonyesha kwa ufanisi pamoja na kutoa taarifa muhimu zinazohusu ulishaji watoto wadogo hususani unyonyeshaji wa maziwa ya mama.
Pamoja na hayo, alisema kuwa, asilimia 49 ya wanawake wanaojifungua ndiyo wanaowaanzishia watoto wao kunyonya maziwa ya mama katika muda sahihi baada ya kujifungua.
“Takribani asilimia 30 ya watoto wachanga wanapewa maji, vinywaji au vyakula kabla hawajaanza kunyonyeshwa na asilimia 50 ya watoto ndio wanaoanzishiwa vyakula vya nyongeza katika umri sahihi wa miezi sita unaopendekezwa kitaalamu,” alisema Wamoja.
Alisema, unyonyeshaji watoto maziwa ya mama unahimizwa kwa sababu ni mlo bora, kamili na muhimu kwa mtoto wa binadamu kuliko chakula kingine katika siku za mwanzo za maisha yake.
Kwa upande wake, mwakilishi kutoka Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFNC), Mary Kibona, alisema ulishaji watoto maziwa ya mama huchangia katika kufikia malengo ya milenia kupunguza umaskini uliokithiri na njaa.
Tanzania inaungana na nchini nyingine duniani kuadhimisha wiki ya unyonyeshaji maziwa ya mama, kuanzia Agosti 1 hadi 7.
 Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Powered by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa