Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Iringa Ramadhan Mungi akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake leo. |
Baadhi ya vifaa vya vinavyotumiwa na Jeshi la Polisi kupima mwendo kasi na kubaini madereva wanaoendesha wakiwa wamelewa. |
Baadhi ya askari wa jeshi la Polisi na waandishi wa habari wakimsikiliza Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa Ramadhan Mungi alipokuwa akiongea na waandishi wa habari. |
Na Gustav Chahe
JESHI la Polisi Mkoani Iringa
limewatahadharisha watu wanaojaribu kupanga mbinu za kusababisha uvunjifu wa
amani katika siku ya kumkumbuka Hayati Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage
Nyerere itakayofanyika kitaifa mkoani Iringa.
Akizungumza na waandishi wa
habari ofisini kwake jana Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa Ramadhan Mungi alisema
jeshi la polisi na vyombo vya usalama kwa ujumla wamejipanga vizuri kuweza
kukabiliana na vitendo vya kihalifu.
Alisema idadi ya askari
imeongezeka kwa kudhibiti vitendo ambavyo vinaweza kusababisha vurugu au
uvunjifu wa amani.
Hata hivyo alisema hali ya
usalama kwa Mkoa wa Iringa ni nzuri kutokana na ulinzi wa vyombo vya usalama na
ulinzi shirikishi uliopo kila kona na kuwatakawale wenye nia ya kuvuruga amani
kuingia katika Mkoa wasijaribu.
“Hali ya usalama kwa Mkoa wetu kwa
ujumla ni nzuri, tumejipanga vizuri kwa ajili ya ulinzi wa wananchi na mali
zao. Maaskari tupo wengi wenye sare na wasio na sare kwa hiyo wananchi wetu
tunawaomba muwe na imani ya usalama” alisema Kamanda Mungi.
Mungi ametoa tahadhari pia kwa
madereva wasiofuata sheria kuwa watashughulikiwa kwa mujibu wa sheria na kwamba
hakutakuwa na msamaha kwa yeyote anayevunja sheria barabarani.
“Wapo madereva vichwa maji
wasiopenda kufuata sheria na wengine kuamua kuvunja sheria kwa makusudi tu. Wapo
wasiopenda kutii amri ya askari barabarani wanaposimamishwa, hao watashughulikiwa
bila huruma” alisema.
Kwamba wapo madereva wanaoendesha
wakiwa wanaongea na simu jambo ambalo kiusalama na sheria za barabarani ni kosa
na kuwataka wananchi kutoa taarifa kwa jeshi la polisi pindi wanapobaini dereva
wa namna hiyo.
Amesema katika kukabiliana na
vitendo vya usalama barabarani, jeshi la polisi lina vifaa maalum kubaini
madereva wazembe na wavunjaji wa sheria na kwamba vifaa hivyo vinauwezo wa
kuona mbali.
“Tuna vifaa vya kutosha kubaini
madereva wanaoendesha wakiwa wamelewa. Dereva yeyote anapoingia Mkoa wa Iringa
ajue hayupo salama kwa sababu tutampata tu hata akiwa mbali” alisema.
Misa ya kumkumbuka Baba wa Taifa
itafanyika katika Kanisa la Moyo Mtakatifu wa Yesu (Kanisa la Kuu la Kiaskofu)
Parokia ya Kihesa Jimbo Katoliki la Iringa ambayo inatarajiwa kuongozwa na Rais
wa Baraza la Maaskofu Tanzania Mhashamu Tarcisius Ngalalekumtwa ambapo baada ya
Misa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete atakwenda
kuhitimisha mbio za Mwenge na kuuzima ambazo zitafanyika kitaifa mkoni Iringa.
NA FRANCIS GODWIN
0 comments:
Post a Comment