Mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa Ritta Kabati akizungumza na wanachama wa VICOBA ambao walifika kupokea fedha alizokuwa amewaahidi |
Baadhi ya wanavikundi vya VICOBA Manispaa ya Iringa walionufaika na fedha za mbunge Kabati
Katibu msaidizi wa mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa Ritta Kabati
, Bw Geofrey Lukuvi akitoa utambulisho wa wageni mbali mbali
katika ukumbi wa Manispaa ya Iringa
Mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa Ritta Kabati akizungumza na
wanachama wa VICOBA ambao walifika kupokea fedha alizokuwa amewaahidi
Katibu wa kikundi cha vijana walioacha kutumia dawa za kulevya
Manispaa ya Iringa Bw Geofrey Lukuvi akipokea msaada wa fedha kutoka
kwa mbunge Ritta Kabati fedha kwa ajili ya kuwawezesha kuongeza mtaji
katika shughuli yao ya utengenezaji Sabuni, wengine pichani ni
mwenyekiti wa CCM Iringa mjini Abed Kiponza ,naibu meya wa Manispaa ya
Iringa Gervas Ndaki
katibu wa timu ya wanawake mkoa wa Iringa Mwanahery Kalolo akipokea
msaada wa mipira kutoka kwa mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa
Ritta Kabati (CCM)
Naibu meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa Bw
Gervas Ndaki aliyekuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo ya mbunge Kabati
kutimiza ahadi zake kwa wanachama wa VICOBA jimbo la Iringa mjini
.......................................................................................................................................................
MBUNGE wa viti maalum kupitia chama cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Iringa Ritta Kabati amewataka wanawake katika jimbo la Iringa mjini kutokubali kuwezeshwa na badala yake kuendelea kujiwezesha kwa kujiunga katika vikundi vya kukopeshana maarufu kama VIKOBA.
Mbunge Kabati alitoa kauli hiyo jana wakati akiwakabidhi msaada wa fedha zaidi ya Tsh milioni 1.8 ambazo ni sehemu ya ahadi zake alizopata kuwaahidi wanachama wa VIKOBA katika jimbo la Iringa mjini.
Alisema kuwa ili kuondokana na kilio cha kuwezeshwa ambacho kimekuwa kikitolewa na wanawake ni vema kuendelea kujiunga katika vikundi vya VIKOBA ambavyo ni ukombozi mkubwa kwao na vinaweza kuwakwamua kiuchumi .
"Lazima wanawake sasa tukatae kuwezeshwa na badala yake tujiwezeshe wenyewe kupitia vikundi kama hivi vya VIKOBA ....mimi kama mbunge wenu nitaendelea kuwa karibu nanyi kwa kuwaunganisha katika vikundi na hata katika taasi za kifedha"
Hata hivyo alisema kuwa moja kati ya jitihada ambazo anaendelea kuzifanya ni pamoja na kuwatafutia uwezeshwaji zaidi wanawake hao ikiwa ni pamoja na kuwaunganisha na benk ya wanawake nchini ili kuja kutoa elimu kabla ya kunufaika na benk hiyo ya wanawake ambayo ni benk kwa ajili ya wanawake wote nchini
Alivitaja vikundi ambavyo amevipatia msaada huo wa fedha kwa kila kikundi kati ya Tsh 200,000 na 250,000 kuwa ni pamoja na kikundi cha vijana walioachana na matumizi ya dawa za kulevya cha Uvimwema,Vicoba Mashine Tatu,Vicoba Azimio ,Vikoba Mtwivila,Kanisa la E.A.G.T Frelimo, Kanisa la Presbyterian,Kanisa la T.A.G Kihesa,Pamoja na wamsanii wa nyimbo za injili watatu
Alisema kuwa vikundi hivyo alipata kuviahidi kwa nyakati tofauti wakati wa ziara yake katika maeneo mbali mbali ya jimbo la Iringa mjini.
Mbali ya kutoa msaada kwa vikundi hivyo pia mbunge huyo na viongozi mbali mbali wa vikundi vya Vicoba na pamoja na mgeni rasmi naibu meya wa Manispaa ya Iringa Gervas Ndaki walimchangia zaidi ya Tsh 200,000 kati ya Tsh 400,000 ambazo mwanafunzi Sillo Ally ambaye anatakiwa kwenda kujiunga na kidato cha tano katika shule ya sekondari ya Songea Boys zinahitajika huku mbunge Kabati akiahidi kumsaidia kumlipia ada baada ya mwanafunzi huyo kudai kunyimwa msaada wa fedha kutoka kwa mbunge wa jimbo la Iringa mjini Mchungaji Peter Msigwa
KWA HISANI YA BLOG YA FRANCIS GODWIN MZEE WA MATUKIO DAIMA
.......................................................................................................................................................
MBUNGE wa viti maalum kupitia chama cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Iringa Ritta Kabati amewataka wanawake katika jimbo la Iringa mjini kutokubali kuwezeshwa na badala yake kuendelea kujiwezesha kwa kujiunga katika vikundi vya kukopeshana maarufu kama VIKOBA.
Mbunge Kabati alitoa kauli hiyo jana wakati akiwakabidhi msaada wa fedha zaidi ya Tsh milioni 1.8 ambazo ni sehemu ya ahadi zake alizopata kuwaahidi wanachama wa VIKOBA katika jimbo la Iringa mjini.
Alisema kuwa ili kuondokana na kilio cha kuwezeshwa ambacho kimekuwa kikitolewa na wanawake ni vema kuendelea kujiunga katika vikundi vya VIKOBA ambavyo ni ukombozi mkubwa kwao na vinaweza kuwakwamua kiuchumi .
"Lazima wanawake sasa tukatae kuwezeshwa na badala yake tujiwezeshe wenyewe kupitia vikundi kama hivi vya VIKOBA ....mimi kama mbunge wenu nitaendelea kuwa karibu nanyi kwa kuwaunganisha katika vikundi na hata katika taasi za kifedha"
Hata hivyo alisema kuwa moja kati ya jitihada ambazo anaendelea kuzifanya ni pamoja na kuwatafutia uwezeshwaji zaidi wanawake hao ikiwa ni pamoja na kuwaunganisha na benk ya wanawake nchini ili kuja kutoa elimu kabla ya kunufaika na benk hiyo ya wanawake ambayo ni benk kwa ajili ya wanawake wote nchini
Alivitaja vikundi ambavyo amevipatia msaada huo wa fedha kwa kila kikundi kati ya Tsh 200,000 na 250,000 kuwa ni pamoja na kikundi cha vijana walioachana na matumizi ya dawa za kulevya cha Uvimwema,Vicoba Mashine Tatu,Vicoba Azimio ,Vikoba Mtwivila,Kanisa la E.A.G.T Frelimo, Kanisa la Presbyterian,Kanisa la T.A.G Kihesa,Pamoja na wamsanii wa nyimbo za injili watatu
Alisema kuwa vikundi hivyo alipata kuviahidi kwa nyakati tofauti wakati wa ziara yake katika maeneo mbali mbali ya jimbo la Iringa mjini.
Mbali ya kutoa msaada kwa vikundi hivyo pia mbunge huyo na viongozi mbali mbali wa vikundi vya Vicoba na pamoja na mgeni rasmi naibu meya wa Manispaa ya Iringa Gervas Ndaki walimchangia zaidi ya Tsh 200,000 kati ya Tsh 400,000 ambazo mwanafunzi Sillo Ally ambaye anatakiwa kwenda kujiunga na kidato cha tano katika shule ya sekondari ya Songea Boys zinahitajika huku mbunge Kabati akiahidi kumsaidia kumlipia ada baada ya mwanafunzi huyo kudai kunyimwa msaada wa fedha kutoka kwa mbunge wa jimbo la Iringa mjini Mchungaji Peter Msigwa
KWA HISANI YA BLOG YA FRANCIS GODWIN MZEE WA MATUKIO DAIMA
0 comments:
Post a Comment