Home » » Polisi Iringa waua jambazi

Polisi Iringa waua jambazi

Mtu mmoja anayetuhumiwa kuwa jambazi ameuawa na mwingine akikamatwa wakati wakivamia duka la Santino Mdesa katika kijiji cha Mkonge kilichopo katika Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa, huku wahamiaji haramu watano kutoka nchi ya Ethiopia wakikamatwa kwa kosa la kuingia nchini pasipo kufuata taratibu.
Akizungumzia tukio hilo ujambazi, kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Iringa ACP Athmani Mungi amesema majambazi hao walifyatua risasi hewani ambapo wananchi walipobaini uwepo wa tukio hilo la Uharifu walizingira eneo hilo ambapo majambazi walitambua mbinu hizo na kukimbia.
Aidha kamanda Mungi amesema wananchi kwa kushirikiana na askari polisi waliwakimbiza majambazi hao na baada ya kuzidiwa nguvu, majambazi walitupa bunduki aina ya SMG iliyokuwa na Lisasi 21, na kisha kutelekeza usafiri wao wa Pikipiki, huku askari wakifanikiwa kumpiga kwa risasi mguuni jambazi mmoja aliyekufa wakati akipelekwa kupata matibabu.
Mungi amesema pia Polisi wamefanikiwa kumkamata mwananchi wa kijiji cha Kitayawa katika Wilaya ya Iringa ambaye amekuwa akitengeneza Bunduki za kienyeji.
Katika tukio lingine kamanda Mungi amesema, wamewakamata wahamiaji haramu watano kutoka nchi ya Ethiopia ambao walikuwa wamejificha katika poli la mashamba ya kijiji cha Mazombe, katika Wilaya ya Kilolo mkoani Iringa, na kuwa wahamiaji hao walikuwa wanaelekea nchini Afrika Kusini.
Akithibitisha kukamatwa kwa wahamiaji hao haramu, ofisa uhamiaji mkoa wa Iringa Ali Nassor amesema wahamiaji hao haramu wakiethiopi wapo chini ya ulinzi kwa hatua zaidi.

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa